WELCOME TORINTO HOT MEDIA BLOG | FOR MORE INFORMATION ABOUT OUR NEWS CONTACT US CELL: +255 756 188 180 | Email: josephlieme@gmail.com| KARIBU TORINTO HOT MEDIA BLOG | KWA MAELEZO ZAIDI KUHUSU HABARI ZETU WASILIANA NASI SIMU: +255 756 188 180 | Barua Pepe: josephlieme@gmail.com | DO YOU NEED TO DEVELOP YOUR BLOG CONTACT US CLICK HERE | JE UNAHITAJI KUBORESHA BLOG YAKO WASILIANA NASI BOFYA HAPA

Jumanne, 14 Novemba 2023

 05:33      No comments

 Torintohot media Blog

Na. Jerome Mlaki wa Dar.



Mjumbe wa halmashauri Kuu ya CCM Taifa Mh. Juma Simba ameendelea na ziara ya kutathimini utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo Ili kubaini mapungufu yaliojitokeza Katika utekelezaji yaweze kufanyiwa Kazi na kuleta maendeleo kwa wananchi.



Ziara hii imelenga kutembelea kata Tisa zilizopo Wilaya ya kigamboni lakini pia kuweka mikakati ya ushindi Katika uchaguzi mdogo kwenye kata ya kimbiji unao unaotarajiwa kufanyika hivi karibuni.



Kata ya somangile  iliyopowilaya ya kigamboni jijini Dar es Salaa m Mh.Juma Simba Gadaffi ameitembelea na kusikiliza changamoto mbali zinazoikabili kata hiyo ikiwemo upinzani mkuu kutoka vyama vya upinzani kwani Ikumbukwe kwamba kata ya somangile iliyopowilaya ya kigamboni ndio makao makuu chadema Katika Wilaya hiyo hivyo chama Cha Mapinduzi Ili kiweze kupata nafasi na Katika kata hiyo hakina budi kijikite Katika utekelezaji wa miradi mbalimbali itakayo leta Imani kwa wananchi.




Mh. Juma Simba amesemaKuwa lazima kila mwanachama ajue wajibu wake na kutekeleza wajibu wake na kusimamia miradi mbalimbali ya maendeleo ndio itakuwa sababu kubwa kwa wananchi kukiamini chama na kukichagua Katika nafasi mbalimbali za uongozi.  



Ziara hii iliambatana na kupokea wanachama wapya wa CCM ikiwemo kupokea Katibu wa Chadema Ndugu Salumu Juma Pazzy  ambaye amerudisha kadi ya Chadema na kujiunga na CCM. 




Pia wanachama wapya kadhaa wameongozwa Katika kiapo Cha kujiunga nachama Cha Mapinduzi pamoja na zoezi la ugawaji wa kadi kwa wanachama hao.



Ikumbukwe kwamba ziara hii inaongozwa na Mwenyekiti wa CCM Taifa Mh Abas Mtemvu ziara ambayo imeleta hamasa na kuchochea umoja kichama na kasi ya utekelezaji wa miradi.


Kata ya Somangile kigamboni Katika ziara hii yalikusanyika matawi kadhaa Ili kuweza kupokea maelekezo kutoka kwa mgeni rasmi matawi hayo ni Kizani, mwenge, Gezs ulole, Malipika, Muongozo, Ndege, Shirikisho, Mboto Kichangani, Mboto mkwajuni, Mwigogo, Sala, Mwanzo Mgumu n.k wenyeviti wa mitaa na viongozi mbalimbali wamehuzuria Katika ziara hii.


0 maoni:

Chapisha Maoni

Kurasa

Translate

Popular Posts

Blog Archive

Tangazo!

JE UNAHITAJI KUBORESHA BLOG YAKO?

WEIGHT MANAGEMENT

WEIGHT MANAGEMENT

SIKILIZA NYIMBO MPYA

Watembeleaji

On Facebook

Tangazo Victoria!!

Date & Time

Weight Management



CLICK THIS IMAGE

Sikiliza Clouds Radio



Sikiliza Kwanza Jamii Radio

Total Pageviews

Fomu ya Anwani

Jina

Barua pepe *

Ujumbe *