WELCOME TORINTO HOT MEDIA BLOG | FOR MORE INFORMATION ABOUT OUR NEWS CONTACT US CELL: +255 756 188 180 | Email: josephlieme@gmail.com| KARIBU TORINTO HOT MEDIA BLOG | KWA MAELEZO ZAIDI KUHUSU HABARI ZETU WASILIANA NASI SIMU: +255 756 188 180 | Barua Pepe: josephlieme@gmail.com | DO YOU NEED TO DEVELOP YOUR BLOG CONTACT US CLICK HERE | JE UNAHITAJI KUBORESHA BLOG YAKO WASILIANA NASI BOFYA HAPA

Jumapili, 30 Agosti 2026



Washington Dc,

Waziri wa Nishati na Makamu wa Rais Mteule, Mhe. Deogratius Ndejembi, amelipongeza Shirika la Kimataifa la Nishati ya Atomiki (IAEA) kwa juhudi zake za kuwezesha uzinduzi wa Mpango wa Teknolojia za Atomiki Zilizopewa Leseni ya Matumizi ya Baharini (ATLAS), akieleza kuwa mpango huo ni hatua muhimu katika kuendeleza teknolojia bunifu za nyuklia na kuongeza matumizi ya nishati ya nyuklia duniani.

Mhe. Ndejembi ameyasema hayo wakati akizungumza katika Mkutano wa Ngazi ya Juu wa Uzinduzi wa ATLAS unaofanyika tarehe 26–27 Agosti 2026 jijini Washington, D.C., Marekani.Amesema mabadiliko makubwa yanayoendelea katika sekta ya nishati duniani yanazilazimu nchi kushirikiana katika kutafuta suluhisho zitakazowezesha kuimarisha usalama wa nishati, kukuza uchumi wa viwanda, kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi na kuhakikisha wananchi wanapata nishati ya uhakika, nafuu na endelevu.

Akieleza hatua zinazochukuliwa na Tanzania katika kuimarisha upatikanaji wa nishati, Mhe. Ndejembi amesema Serikali inaendelea kutekeleza mkakati wa kutumia mchanganyiko wa vyanzo mbalimbali vya nishati, ikiwemo umeme wa maji, gesi asilia, jua, upepo na vyanzo vingine vya nishati jadidifu.

Ameongeza kuwa Tanzania inaendelea kufuatilia kwa karibu maendeleo ya teknolojia bunifu za nishati, ikiwemo teknolojia za nyuklia, kwa lengo la kuongeza fursa za upatikanaji wa nishati salama, ya uhakika na endelevu pamoja na kuchochea maendeleo ya kiuchumi na kijamii.

Na. Jerome Mlaki wa Dar.

Bodi ya Ligi Kuu Tanzania (TPLB) imetangaza kuwa msimu wa Ligi ya NBC Championship kwa mwaka 2026/2027 unatarajiwa kuanza rasmi Oktoba 29, 2026 na kukamilika Mei 27, 2027.

Hayo yamesemwa Agosti 28, 2026, jijini Dar es Salaam na Afisa Mtendaji Mkuu wa TPLB, Cornel Barnabas, wakati akizungumza kuhusu maandalizi ya msimu mpya wa ligi hiyo.

Barnabas amesema ratiba ya msimu huo imeandaliwa kwa kutumia mfumo wa kidijitali, hatua inayolenga kuwezesha upangaji wa michezo kuwa wenye ufanisi na kuzingatia mahitaji ya mashindano.

“Ratiba imeandaliwa kidijitali, hivyo nazitakia maandalizi mema timu zote zitakazoshiriki katika mtanange huo,” amesema Barnabas.

Kutangazwa kwa tarehe ya kuanza kwa msimu huo kunazipa klabu zinazoshiriki NBC Premier League nafasi ya kuendelea na maandalizi kuelekea msimu mpya, huku mashabiki wa soka nchini wakisubiri kwa hamu kuanza kwa ushindani mwingine wa kuwania ubingwa.

Kwa mujibu wa taarifa zilizotolewa kuhusu ratiba ya msimu wa 2026/2027, NBC Premier League inaendelea kuwa miongoni mwa mashindano yanayofuatiliwa kwa karibu katika soka la Tanzania.

Kwa upande wake,Afisa Habari wa TPLB, Yahaya Abusheh, amesema msimu huo utashirikisha jumla ya timu 16, ambazo zitagawanywa katika makundi mawili.

Amesema kundi A litakuwa na timu nane, huku kundi B likiwa na timu nane


Na Jerome Mlaki wa Dar.

DAR ES SALAAM: 

Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam linawashikilia watu 11, akiwemo Timothy Eshemo maarufu kwa jina la Jack, kwa tuhuma za kuiba miundombinu ya Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL).

Taarifa hiyo imetolewa Agosti 27, 2026 na Kamanda wa Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, SACP Jumanne Muliro, wakati akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam.

SACP Muliro amesema baadhi ya watuhumiwa hao wanadaiwa kujihusisha na kupanga uhalifu, kuiba pamoja na kununua miundombinu hiyo kwa lengo la kufanya biashara.

Amesema miundombinu inayodaiwa kuibwa ni pamoja na nyaya za shaba (copper cables), ambazo zimekuwa zikisababisha kukatika au kuathiriwa kwa huduma za mawasiliano katika taasisi mbalimbali za Serikali na binafsi.“Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam linalaani hujuma hizi na litawashughulikia wale wote wanaohusika kupanga na kuiba miundombinu hiyo,” amesema SACP Muliro.

Kwa mujibu wa Kamanda Muliro, zoezi la kuwabaini na kuwakamata watuhumiwa hao limefanyika kuanzia Juni hadi Agosti 2026 kwa kushirikiana na Kitengo cha Usalama cha TTCL.

Amesema baadhi ya watuhumiwa walitumia mbinu ya kujifanya wafanyakazi wa TTCL ili kupata nafasi ya kufikia miundombinu hiyo na kuiba nyaya zenye shaba.

“Uhalifu umefanyika katika maeneo ya Kinondoni, Upanga na Mikocheni, ambapo watuhumiwa hao walikuwa wanaongozwa na mtu anayejulikana kwa jina la Timothy Eshemo maarufu kama ‘Jack’,” amesema SACP MuliroJeshi la Polisi limeendelea na uchunguzi ili kubaini mtandao mzima wa watu wanaodaiwa kuhusika na wizi huo pamoja na hatua nyingine za kisheria dhidi ya watuhumiwa.

Katika hatua nyingine Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es salaam limesema kuwa hali ya usalama inaendelea vizuri huku likitoa wito kwa Wananchi kuendelea kutoa ushirikiano kwa Jeshi hilo ili kukomesha vitendo vya uhalifu.

Alhamisi, 2 Aprili 2026

Torintohot 

Na Jerome mlaki 0789106710


Maadhimisho ya Siku ya Ukombozi wa Afrika yanatarajiwa kufanyika leo jijini Dar es Salaam.

Akizungumza wakati wa kufungua mdahalo uliofanyika katika Kituo cha Urithi wa Ukombozi wa Afrika, Mkurugenzi Msaidizi wa Utamaduni na Maadili ya Taifa, Dkt. Julieth Kabyemela, amesema kuwa Tanzania ni moja ya nchi yenye kumbukumbu nyingi kuhusu harakati za ukombozi barani Afrika.

“Sisi kama Watanzania, siku hii ni muhimu sana kwetu, kwa sababu nchi yetu ilikuwa kitovu cha harakati za kupigania uhuru wa mataifa mbalimbali ya Afrika,” amesema Dkt. Kabyemela.

Naye Mratibu wa Kituo hicho, Christopher Mhongole, amesema kuwa nchi nyingi za Afrika zinaweza kujifunza historia ya ukombozi kwa ushahidi wa kutosha kwa kuitembelea Tanzania, ambako harakati nyingi ziliratibiwa.

“Hivyo basi, maadhimisho kama haya ni muhimu kwa Tanzania, kwani hutoa fursa ya kuielimisha jamii, hasa vijana, ili watambue na kuthamini historia ya nchi yao,” amesema Mhongole.

Aidha, mmoja wa wanafunzi wa kidato cha sita kutoka Shule ya Sekondari Zanaki, jijini Dar es Salaam, Jesca Denis Monahera, aliyeshiriki katika mdahalo huo, amesema kuwa jambo la kwanza alilojifunza ni umuhimu wa kuwa mzalendo kwa nchi yake

Jumatatu, 30 Machi 2026

 Torintohot 

By Jerome mlaki 0789106710


AND FIFTY MAGENDELA, KARATU

FARMERS in the Arusha region who have received training in ecological farming have demonstrated in practice that Tanzania can move away from the use of pesticides and industrial fertilizers.


According to George Ndege, who is among the Ecological Agriculture farmers, Karatu in Arusha region, he notes that Ecological Agriculture, which uses natural, non-industrial inputs, has had significant health benefits for consumers and land protection in light of climate change.


Mzee Ndege says that on his 10-acre plot of land, he has been cultivating vegetables, coffee and beekeeping and is proud that the vegetables he grows have been in greater demand because they are better than those grown using industrial fertilizers.


 "Here I grow vegetables, coffee using natural fertilizers and pesticides by making them myself and making them safer for the consumer unlike those grown with pesticides and industrial fertilizers. He says his main market after harvesting is in tourist hotels in Karatu in Arusha region and it has given him great success including increasing his income and building some guest houses in Karatu."


He also notes that he has been confident of the market although he is unable to explain it because the demand is high as he currently serves only five hotels despite the presence of more than 80 tourist hotels in the area.


Meanwhile, Elder Modest Fantee, a farmer from Endagem village, Karatu in Arusha region, has made it clear that through ecological farming he has been obtaining abundant crops without using farming that has an impact on the land.


I received my Ecological Agriculture education from the IDP Institute, which has been a great help to us as they provide us with natural seeds and have developed a system for keeping seed banks in villages and here I have a seed bank and they are protected in a natural way. “By using Ecological agriculture, my family also has enough food with good nutrition since its growth was not done with chemical fertilizers, here I use cow manure and natural fertilizers that I make myself.


"I am also grateful that after we started using Ecological Agriculture, we have also started teaching many people and for us we have become like a classroom, so this education continues to spread to other areas within our ward and outside," he said.


Also, Adili Msangi who is involved in ecological agriculture, animal husbandry, production of organic fertilizers and natural pesticides and conservation of natural seeds, in Karatu district, confirms that using sustainable agricultural systems has helped them to have safe crop production for human consumption and environmental protection.

In fact, ecological agriculture has helped us to give good results on the land by obtaining safe crops as we use natural fertilizers made from animal bones, as well as crop residues which others see as garbage and we transform them into a working tool and give good results on the farm.

 "We also use cow urine which we compost and at the end of the day it becomes a pesticide and that has been attracting many farmers to come and train and use it in their fields and abandon chemical pesticides. "We use natural pesticides and fertilizers to ensure that we get safe crops for human consumption but also Ecological agriculture does not kill insects but repels them but if you use industrial ones they kill all insects including those that pollinate flowers including bees and butterflies, he said.

He said that since he received his agricultural ecology education in 2017, he has had great success in the field and a wide scope for distributing natural seeds to other farmers, although the biggest challenge he faces is the lack of a bone processing machine for making fertilizer, which costs 12 million.

 Torintohot

By Jerome Mlaki 0789106710

And Our Writer.

Chinese-owned Fortune Paper Group, which has invested more than 154 billion shillings in Tanzania since 2022, is seeking policy support from the government to protect its recycling-based manufacturing business from what it calls unfair competition from cheap imported products.

In a special interview held on the sidelines of the International Zero Waste Day exhibition held at Mnazi Mmoja grounds, the company said it plans to expand production and strengthen its long-term investment in Tanzania, which currently employs more than 150 local workers.

The exhibition was held today, March 30, 2026 in Dar es Salaam as part of the culmination of the national celebrations of the International Zero Waste Day and was attended by the Minister of State in the Office of the Vice President responsible for the Environment, Hon. Hamad Yusuf Masauni.

Speaking, Fortune Paper Factory Business Manager, Colin Yang, said the company collects waste paper from various locations in Tanzania and converts it into packaging products used for boxes, envelopes and other industrial uses.

"This is our raw material, we collect waste paper from all over the country and convert it into products for various types of packaging," said Yang.

Describing the investment as a business as well as a contribution to the environmental sustainability agenda in Tanzania.

The company began operations in Tanzania in 2022 and has since invested more than $60 million in factory production capacity and local operations, according to Yang.

He also added that the Fortune Paper factory intends to expand its products as well as increase capital investment due to expectations of long-term growth in domestic demand.

However, Yang said the business is facing pressure from imported paper products, especially from India and China, which he said are entering the Tanzanian market under a duty exemption scheme that allows them to avoid taxes paid by local producers.

Jumamosi, 14 Machi 2026

 Kamati hiyo imetoa Rai kwa Wizara ya Nishati na TANESCO  inaendelea kuendelea na  mikakati ya kuanza utekelezaji wa awamu ya pili ya mradi huo ili kuongeza zaidi uwezo wa uzalishaji wa umeme Nchini.


Na Jerome Mlaki 0789106710


📌 Watembelea mradi kuona ufanisi wake

📌 Shilingi bilioni 118 zatumika kutekeleza mradi

📌 Watoa rai awamu ya pili kuanza kwa kasi

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini imelipongeza Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) kwa usimamizi na utekelezaji mzuri wa Mradi wa Uzalishaji Umeme kwa nguvu ya Jua wa Kishapu wenye uwezo wa Megawati 50 unaotekelezwa katika Mkoa wa Shinyanga.

Pongezi hizo zimetolewa na Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Mhe. Subira Mgallu, mara baada ya Kamati kutembelea mradi huo tarehe 13 Machi, 2026 kwa lengo la kujionea maendeleo ya utekelezaji wake pamoja na ufanisi wa matumizi ya fedha zilizotolewa na Serikali.

Akizungumza mara baada ya ziara hiyo, Mhe. Mgallu alisema mradi huo ni hatua muhimu katika mageuzi ya sekta ya nishati nchini kutokana na matumizi ya teknolojia ya nishati jadidifu.“Tumetembelea mradi huu wa uzalishaji wa umeme kwa kutumia teknolojia ya jua na tunaona ni mapinduzi makubwa katika sekta ya nishati nchini. Hii ni hatua muhimu kwani kwa mara ya kwanza Tanzania inapata Megawati 50 za umeme kutoka kwenye nishati ya jua,” alisema Mhe. Mgallu.

Alisema Kamati imeridhishwa na namna fedha zilizotolewa na Serikali kwa ajili ya utekelezaji wa mradi huo zimetumika ipasavyo na kufanikisha utekelezaji wa mradi huo kwa ufanisi.

“Kama Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini, tumeridhishwa na matumizi ya fedha zilizotolewa na Serikali kwa ajili ya mradi huu. Tunaona wazi kuwa fedha hizo zimetumika vizuri katika utekelezaji wa mradi huu wenye thamani ya takribani shilingi bilioni 118,” alieleza.Aidha, alisema mradi huo tayari umeanza kuchangia Megawati 50 katika Mfumo wa Gridi ya Taifa, hatua inayochangia kuongeza uwezo wa uzalishaji wa umeme nchini pamoja na kuimarisha vyanzo mseto vya nishati.

“Utekelezaji wa mradi huu unaonesha dhamira ya Serikali ya kuhakikisha kunakuwa na vyanzo mbalimbali vya kuzalisha umeme. Hii inaongeza uhakika wa upatikanaji wa nishati ya umeme nchini,” alisema.Kwa upande wake, Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi, alisema mradi wa Kishapu unatekelezwa kwa awamu mbili ambapo awamu ya kwanza ya Megawati 50 tayari imekamilika na imeanza kuingiza umeme katika Gridi ya Taifa.

“Mradi huu una awamu mbili ambapo awamu ya kwanza ya Megawati 50 tayari imekamilika na imeanza kuingiza umeme kwenye Gridi ya Taifa. Awamu ya pili itahusisha uzalishaji wa Megawati 100 zaidi na kufanya jumla ya Megawati 150 kutoka katika mradi huu,” alisema Mhe. Ndejembi.

Kamati hiyo imetoa Rai kwa Wizara ya Nishati na TANESCO  inaendelea kuendelea na  mikakati ya kuanza utekelezaji wa awamu ya pili ya mradi huo ili kuongeza zaidi uwezo wa uzalishaji wa umeme Nchini.

  

 Na Jerome Mlaki

Dar es Salaam 

Waziri Mkuu Mstaafu, Mheshimiwa Kassim Majaliwa,Leo amewafuturisha mamia ya waumini wa dini ya kiislam pamoja na viongozi katika tukio maalum la Iftar lililofanyika leo Machi 10, 2025 jijini Dar es Salaam katika Hoteli ya Serena. 

Tukio hilo limeandaliwa na Mshauri wa Rais na Waziri Mkuu Mstaafu, Mheshimiwa Kassim Majaliwa.

Tukio hilo la Iftar limewakutanisha viongozi mbalimbali wa Serikali, viongozi wa dini, wadau kutoka sekta binafsi pamoja na wageni wengine mashuhuri waliokusanyika kwa ajili ya kushiriki futari na kuimarisha mshikamano na upendo katika kipindi hiki cha Mwezi Mtukufu wa Ramadhani.

Hata hivyo katika tukio hilo walihudhuria makundi mbalimbali ya kijamii wakiwemo watoto wanaoishi katika mazingira magumu 

Waumini wa dini ya kiislamu duniani kote wapo katika kipindi Cha Mwezi mtukufu wa Ramadhan.

 Na Jerome mlaki 0789106710

 




Kuelekea maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani, Chama cha ACT Wazalendo kupitia Ngome yake ya Wanawake kimezindua mnara wa kumbukumbu kwa ajili ya watu waliopoteza maisha kufuatia matukio ya vurugu yaliyotokea Oktoba 29, 2025.


Akizungumza wakati wa uzinduzi huo uliofanyika Machi 3, 2026, Kiongozi wa Chama cha ACT Wazalendo, Dorothy Semu, amesema hatua hiyo inalenga kuenzi kumbukumbu ya waliopoteza maisha na kuonesha mshikamano na familia zilizoathirika na matukio hayo.


Dorothy amesema maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani ni wakati muhimu wa kutafakari nafasi ya wanawake katika jamii pamoja na changamoto wanazokutana nazo, ikiwemo maumivu wanayopitia mama waliopoteza watoto wao katika matukio hayo.


“Machozi ya mama anayesubiri kurejeshewa mwili wa mwanae ni kilio kisicho na sauti, lakini chenye uzito mkubwa kwa taifa. Machozi ya mama ni deni la taifa,” amesema Dorothy.


Amesisitiza kuwa taifa linahitaji uponyaji wa kweli kufuatia matukio ya Oktoba 29, akieleza kuwa uponyaji huo unaweza kupatikana kwa kukabiliana na ukweli wa yaliyotokea pamoja na kuhakikisha haki inapatikana kwa waathirika.


Aidha, amelani vikali vitendo vya ukiukwaji wa haki za binadamu vilivyofanywa dhidi ya Watanzania na kusisitiza umuhimu wa kusikiliza sauti za waathirika badala ya kuficha ukweli.


Dorothy pia ametoa wito wa kuundwa kwa tume huru ya uchunguzi iliyo nje ya Serikali ili kuchunguza kwa kina matukio hayo, akisema hatua hiyo ni muhimu katika kuhakikisha haki, uwajibikaji na maridhiano ya kweli kwa taifa.

 Na Jerome mlaki 0789106710



Na Torintohot 

Dar es Salaam leo imekuwa mwenyeji wa mkutano wa Tume ya Kudumu ya Pamoja (Joint Permanent Commission - JPC) kati ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Jamhuri ya Uganda, mkutano unaolenga kuimarisha zaidi uhusiano wa kidiplomasia na ushirikiano kati ya mataifa hayo mawili jirani.

Mkutano huo umefunguliwa rasmi na Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Samwel Shelukindo, ambaye amesisitiza umuhimu wa jukwaa hilo kama sehemu muhimu ya kuimarisha mahusiano ya pande mbili pamoja na kupanua ushirikiano katika sekta mbalimbali.

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa mkutano huo, Balozi Shelukindo amesema kuwa Tume ya Kudumu ya Pamoja inatoa fursa muhimu kwa nchi hizo mbili kufanya mazungumzo yenye kujenga, kupitia maendeleo ya ushirikiano uliopo, pamoja na kubaini maeneo mapya ya ushirikiano yatakayowanufaisha wananchi wa Tanzania na Uganda.

Aidha, mkutano huo unawakutanisha maafisa waandamizi wa serikali kutoka Tanzania na Uganda kwa lengo la kupitia utekelezaji wa makubaliano yaliyofikiwa katika mikutano iliyopita ya JPC pamoja na kujadili namna bora ya kuimarisha ushirikiano katika sekta mbalimbali ikiwemo biashara, miundombinu, nishati na usafirishaji.

Vilevile, majadiliano yanatarajiwa kujikita katika kutafuta suluhu za changamoto zinazoweza kuathiri biashara ya mipakani kati ya nchi hizo mbili, ikiwemo kuondoa vikwazo vya ushuru na visivyo vya ushuru ili kurahisisha biashara na kuongeza fursa za kiuchumi kwa wananchi wa Tanzania na Uganda

Kurasa

Translate

Popular Posts

Blog Archive

Tangazo!

JE UNAHITAJI KUBORESHA BLOG YAKO?

WEIGHT MANAGEMENT

WEIGHT MANAGEMENT

SIKILIZA NYIMBO MPYA

Watembeleaji

On Facebook

Tangazo Victoria!!

Date & Time

Weight Management



CLICK THIS IMAGE

Sikiliza Clouds Radio



Sikiliza Kwanza Jamii Radio

Total Pageviews

Fomu ya Anwani

Jina

Barua pepe *

Ujumbe *