WELCOME TORINTO HOT MEDIA BLOG | FOR MORE INFORMATION ABOUT OUR NEWS CONTACT US CELL: +255 756 188 180 | Email: josephlieme@gmail.com| KARIBU TORINTO HOT MEDIA BLOG | KWA MAELEZO ZAIDI KUHUSU HABARI ZETU WASILIANA NASI SIMU: +255 756 188 180 | Barua Pepe: josephlieme@gmail.com | DO YOU NEED TO DEVELOP YOUR BLOG CONTACT US CLICK HERE | JE UNAHITAJI KUBORESHA BLOG YAKO WASILIANA NASI BOFYA HAPA

Jumamosi, 14 Machi 2026

 Kamati hiyo imetoa Rai kwa Wizara ya Nishati na TANESCO  inaendelea kuendelea na  mikakati ya kuanza utekelezaji wa awamu ya pili ya mradi huo ili kuongeza zaidi uwezo wa uzalishaji wa umeme Nchini.


Na Jerome Mlaki 0789106710


📌 Watembelea mradi kuona ufanisi wake

📌 Shilingi bilioni 118 zatumika kutekeleza mradi

📌 Watoa rai awamu ya pili kuanza kwa kasi

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini imelipongeza Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) kwa usimamizi na utekelezaji mzuri wa Mradi wa Uzalishaji Umeme kwa nguvu ya Jua wa Kishapu wenye uwezo wa Megawati 50 unaotekelezwa katika Mkoa wa Shinyanga.

Pongezi hizo zimetolewa na Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Mhe. Subira Mgallu, mara baada ya Kamati kutembelea mradi huo tarehe 13 Machi, 2026 kwa lengo la kujionea maendeleo ya utekelezaji wake pamoja na ufanisi wa matumizi ya fedha zilizotolewa na Serikali.

Akizungumza mara baada ya ziara hiyo, Mhe. Mgallu alisema mradi huo ni hatua muhimu katika mageuzi ya sekta ya nishati nchini kutokana na matumizi ya teknolojia ya nishati jadidifu.“Tumetembelea mradi huu wa uzalishaji wa umeme kwa kutumia teknolojia ya jua na tunaona ni mapinduzi makubwa katika sekta ya nishati nchini. Hii ni hatua muhimu kwani kwa mara ya kwanza Tanzania inapata Megawati 50 za umeme kutoka kwenye nishati ya jua,” alisema Mhe. Mgallu.

Alisema Kamati imeridhishwa na namna fedha zilizotolewa na Serikali kwa ajili ya utekelezaji wa mradi huo zimetumika ipasavyo na kufanikisha utekelezaji wa mradi huo kwa ufanisi.

“Kama Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini, tumeridhishwa na matumizi ya fedha zilizotolewa na Serikali kwa ajili ya mradi huu. Tunaona wazi kuwa fedha hizo zimetumika vizuri katika utekelezaji wa mradi huu wenye thamani ya takribani shilingi bilioni 118,” alieleza.Aidha, alisema mradi huo tayari umeanza kuchangia Megawati 50 katika Mfumo wa Gridi ya Taifa, hatua inayochangia kuongeza uwezo wa uzalishaji wa umeme nchini pamoja na kuimarisha vyanzo mseto vya nishati.

“Utekelezaji wa mradi huu unaonesha dhamira ya Serikali ya kuhakikisha kunakuwa na vyanzo mbalimbali vya kuzalisha umeme. Hii inaongeza uhakika wa upatikanaji wa nishati ya umeme nchini,” alisema.Kwa upande wake, Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi, alisema mradi wa Kishapu unatekelezwa kwa awamu mbili ambapo awamu ya kwanza ya Megawati 50 tayari imekamilika na imeanza kuingiza umeme katika Gridi ya Taifa.

“Mradi huu una awamu mbili ambapo awamu ya kwanza ya Megawati 50 tayari imekamilika na imeanza kuingiza umeme kwenye Gridi ya Taifa. Awamu ya pili itahusisha uzalishaji wa Megawati 100 zaidi na kufanya jumla ya Megawati 150 kutoka katika mradi huu,” alisema Mhe. Ndejembi.

Kamati hiyo imetoa Rai kwa Wizara ya Nishati na TANESCO  inaendelea kuendelea na  mikakati ya kuanza utekelezaji wa awamu ya pili ya mradi huo ili kuongeza zaidi uwezo wa uzalishaji wa umeme Nchini.

  

 Na Jerome Mlaki

Dar es Salaam 

Waziri Mkuu Mstaafu, Mheshimiwa Kassim Majaliwa,Leo amewafuturisha mamia ya waumini wa dini ya kiislam pamoja na viongozi katika tukio maalum la Iftar lililofanyika leo Machi 10, 2025 jijini Dar es Salaam katika Hoteli ya Serena. 

Tukio hilo limeandaliwa na Mshauri wa Rais na Waziri Mkuu Mstaafu, Mheshimiwa Kassim Majaliwa.

Tukio hilo la Iftar limewakutanisha viongozi mbalimbali wa Serikali, viongozi wa dini, wadau kutoka sekta binafsi pamoja na wageni wengine mashuhuri waliokusanyika kwa ajili ya kushiriki futari na kuimarisha mshikamano na upendo katika kipindi hiki cha Mwezi Mtukufu wa Ramadhani.

Hata hivyo katika tukio hilo walihudhuria makundi mbalimbali ya kijamii wakiwemo watoto wanaoishi katika mazingira magumu 

Waumini wa dini ya kiislamu duniani kote wapo katika kipindi Cha Mwezi mtukufu wa Ramadhan.

 Na Jerome mlaki 0789106710

 




Kuelekea maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani, Chama cha ACT Wazalendo kupitia Ngome yake ya Wanawake kimezindua mnara wa kumbukumbu kwa ajili ya watu waliopoteza maisha kufuatia matukio ya vurugu yaliyotokea Oktoba 29, 2025.


Akizungumza wakati wa uzinduzi huo uliofanyika Machi 3, 2026, Kiongozi wa Chama cha ACT Wazalendo, Dorothy Semu, amesema hatua hiyo inalenga kuenzi kumbukumbu ya waliopoteza maisha na kuonesha mshikamano na familia zilizoathirika na matukio hayo.


Dorothy amesema maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani ni wakati muhimu wa kutafakari nafasi ya wanawake katika jamii pamoja na changamoto wanazokutana nazo, ikiwemo maumivu wanayopitia mama waliopoteza watoto wao katika matukio hayo.


“Machozi ya mama anayesubiri kurejeshewa mwili wa mwanae ni kilio kisicho na sauti, lakini chenye uzito mkubwa kwa taifa. Machozi ya mama ni deni la taifa,” amesema Dorothy.


Amesisitiza kuwa taifa linahitaji uponyaji wa kweli kufuatia matukio ya Oktoba 29, akieleza kuwa uponyaji huo unaweza kupatikana kwa kukabiliana na ukweli wa yaliyotokea pamoja na kuhakikisha haki inapatikana kwa waathirika.


Aidha, amelani vikali vitendo vya ukiukwaji wa haki za binadamu vilivyofanywa dhidi ya Watanzania na kusisitiza umuhimu wa kusikiliza sauti za waathirika badala ya kuficha ukweli.


Dorothy pia ametoa wito wa kuundwa kwa tume huru ya uchunguzi iliyo nje ya Serikali ili kuchunguza kwa kina matukio hayo, akisema hatua hiyo ni muhimu katika kuhakikisha haki, uwajibikaji na maridhiano ya kweli kwa taifa.

 Na Jerome mlaki 0789106710



Na Torintohot 

Dar es Salaam leo imekuwa mwenyeji wa mkutano wa Tume ya Kudumu ya Pamoja (Joint Permanent Commission - JPC) kati ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Jamhuri ya Uganda, mkutano unaolenga kuimarisha zaidi uhusiano wa kidiplomasia na ushirikiano kati ya mataifa hayo mawili jirani.

Mkutano huo umefunguliwa rasmi na Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Samwel Shelukindo, ambaye amesisitiza umuhimu wa jukwaa hilo kama sehemu muhimu ya kuimarisha mahusiano ya pande mbili pamoja na kupanua ushirikiano katika sekta mbalimbali.

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa mkutano huo, Balozi Shelukindo amesema kuwa Tume ya Kudumu ya Pamoja inatoa fursa muhimu kwa nchi hizo mbili kufanya mazungumzo yenye kujenga, kupitia maendeleo ya ushirikiano uliopo, pamoja na kubaini maeneo mapya ya ushirikiano yatakayowanufaisha wananchi wa Tanzania na Uganda.

Aidha, mkutano huo unawakutanisha maafisa waandamizi wa serikali kutoka Tanzania na Uganda kwa lengo la kupitia utekelezaji wa makubaliano yaliyofikiwa katika mikutano iliyopita ya JPC pamoja na kujadili namna bora ya kuimarisha ushirikiano katika sekta mbalimbali ikiwemo biashara, miundombinu, nishati na usafirishaji.

Vilevile, majadiliano yanatarajiwa kujikita katika kutafuta suluhu za changamoto zinazoweza kuathiri biashara ya mipakani kati ya nchi hizo mbili, ikiwemo kuondoa vikwazo vya ushuru na visivyo vya ushuru ili kurahisisha biashara na kuongeza fursa za kiuchumi kwa wananchi wa Tanzania na Uganda





Torintohot 

Na. Jerome Mlaki. 0789106710

Kampuni ya ZERA imezindua magari yake mapya aina ya ZERA ZMEV ambayo yanatumia nishati ya umeme.

Akizungumza katika uzinduzi wa magari hayo, Katibu Mkuu Wizara ya Nishati anayeshughulikia nishati, Mhandisi Felichism Mramba, amempongeza ujio wa magari hayo ya umeme kwa sasa kwa kiwango kikubwa na kusema kuwa utaleta mapinduzi katika eneo la huduma za usafirishaji hapa nchini.

Mhandisi Mramba amesema kwa makadirio kwa sasa nchini kuna magari zaidi ya elfu 5 yanayotumia nishati ya umeme, hivyo ujio wa magari ya ZERA si tu utasaidia sekta ya usafirishaji bali pia itakuza vipato vya Watanzania.

Amesema gharama za kuendesha chombo hicho cha umeme kunapunguza gharama kwa zaidi ya asilimia 85.

"Gari hizi ambazo zinaweza kutembea kilomota 300 baada ya kuchaji ni hatua kubwa ya mafanikio na itaboresha mazingira kwani magari hayo hayatoi moshi," alisema.

Amesema vyombo vinavyotumia nishati ya umeme ni mwaroabaini ambao utaifanya Wizara ya Nishati kuongeza uzalishaji wa umeme ili kuendana na kasi ya teknolojia hii ikiwa ni pamoja na kuweka maeneo maalum ya kuchaji magari hayo ambapo magari mengine yatachajiwa kwa wakati mmoja.

"nataka niwahakikishie kwamba itapunguza sana ukali wa maisha lakini kwa kuagiza gari hizi ambazo gharama ni wakati tu wa kuagiza ila baada ya hapo hazibadikishwi oil wala kuhitaji matengenezo ya mara kwa mara," aliongeza Mramba.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya ZERA, Emmanuel Kazimoto, amesema kampuni hiyo inalenga kujenga mfumo kamili wa usafiri wa umeme unaojumuisha uuzaji wa magari, ufungaji wa miundombinu ya kuchaji, ushauri wa kubadilisha magari ya kampuni kuwa ya vanema, pamoja na huduma za matengenezo.

Ameeleza mpango wao utaanza kwa kuingiza nchini magari ya kampuni hiyo ya ZERA yaliyokamilika (CBU), kisha hatua ya pili italenga kuingiza yaliyoandaliwa nusu (SDU) ili kuongeza ushiriki wa wataalamu wa ndani, huku hatua ya tatu ikilenga kuanzisha mkusanyiko wa magari hayo hapa nchini.

Aidha amesema magari hayo yametoka China lakini baadaye wataanza kutengeneza hapa nchini kwani tayari wameshapata kibali kutoka TISEZA cha kuyatengeneza nchini na kiwanda chake kitakuwa eneo la Kibaha, Pwani.

Amesema katika hatua za mwanzo, kampuni hiyo imeingiza magari kadhaa ya umeme kwa ajili ya maonesho na matumizi ya majaribio, ikiwa ni pamoja na yale ya abiria na mabasi madogo yanayoweza kutumika katika usafiri wa mjini. Mpango huo pia unatekelezwa kwa ushirikiano na wadau mbalimbali ikiwemo Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) katika masuala ya nishati na miundombinu 

karibu kwa matangazo mbalimbali kwa b bei nafuu sana

Alhamisi, 14 Desemba 2023

Digital Online

Torintohot media Blog 

Na Jerome Mlaki, DSM.













 .

Akizungaumza na waandishi wa habari pamoja na wadau wa sekta binafsi na waalikwa Katika kikao hichi Afisa Mtendaji Mkuu (PPRA).Mh. Eliakim Maswi amesema kuwa mfumo huu wa ununuzi unaojulikana kwa Jina la Nest utasaidia Sana kuweka wazi Namna utendaji wa shughuli za mauziano zinavyoenda na hivyo kuziba mianya ambayo ingeweza kujitokeza kutokana na ukosefu wa mfumo huu.


Aidha Mh. Eliakim Maswi Asema kuwa mfumo huu wa ununuzi wa umma umekuja kwa lengo la kuraisisha utekelezaji mbalimbali wa shughuli za kibiashara na Tena kwa uwazi zaidi ambapo washiriki wote wa manunuzi wataweza Fanya shughuli kwa Mazingira yalioboreshwa Katika mfumo wa kidigilitali.


Faida ya kwanza ya mfumo huu wa ununuzi wa umma ni kuongezeka kwa uwazi zaidi ambapo washiriki wa biashara wataweza kufanya biashara Katika mazingira ambayo ambayo watu mbalimbali Wanaona mwanzo mwisho. 



Faida ya pili kuongezeka kwa uwajibikaji watumishi wa idara wataweza kuonekana utekelezaji wao wa Kazi hivyo inapunguza uzembe Katika utekelezaji wa Mfumo.




Mh. Eliakim Maswi amesema kuwa mfumo huu wa ununuzi unaojulikana kwa Jina la Nest utasaidia Sana kuweka wazi Namna utendaji wa shughuli za mauziano zinavyoenda na hivyo kuziba mianya ambayo ingeweza kujitokeza kutokana na ukosefu wa mfumo huu.


Faida nyingine ni urahisi wa kupata taarifa na Tena zilizo sahihi, mfumo huu unarahisisha Kazi zifanyike kwa wakati na upatikanaji wa taarifa za Kazi hata mtu akiwa mbali Bado anaouwezo wa kujua kinachoendelea..amesema Mh. Maswi. .

Jumatano, 13 Desemba 2023

 Jumatano, Novemba 13, 2023

Digital online 

Torintohot media Blog.

Na. Jerome Mlaki wa Dar

Mtakwimu Mkuu wa Serikali, Salum Kassim Ali akizungumza katika kikao cha usambazaji na matumizi ya matokeo ya viashiria vya Sensa ya watu na makaazi ya mwaka 2022 ngazi ya Mkoa, Ziwani Mjini Unguja.



  • Imeelezwa kuwa taarifa zinazotolewa na wananchi ndizo zinaiwezesha Serikali kubadilisha hali zao za maisha kwa kuwaletea maendeleo.
  • Unguja. Mtakwimu Mkuu wa Serikali Zanzibar, Salum Kassim Ali amesema taarifa zinazotolewa na wananchi ndizo zinazoiwezesha Serikali kubadilisha hali zao za maisha kwa kuwaletea maendelo.Akizungumza hayo leo, Novemba 13, katika kikao cha usambazaji na matumizi ya matokeo ya viashiria vya Sensa ya watu na makazi ya mwaka 2022 Polisi Ziwani, ameeleza kuwa kuna kila sababu ya wananchi kupatiwa uwelewa wa umuhimu wa kutoa taarifa sahihi ili kuweka mipango madhubuti katika upatikanaji wa huduma.

"Matokeo ya Sensa ni muhimu kwani yanasaidia kupanga, kusimamia na kubadilisha maisha ya wananchi na kuwaweka katika hali nzuri," amesema Salum.




Mtakwimu huyo, alibainisha kuwa takwimu ya idadi ya watu na makazi itasaidia kusimamia mchakato wa kutoa huduma ikiwemo huduma za afya kwa wananchi kwani lengo ni kuongeza ufanisi wa maendeleo nchini.

Mkuu wa Mkoa Mjini Magharibu, Idrissa Kitwana Mustafa amesema iwapo matokeo hayo yatatumika vizuri basi ni wazi kuwa jamii itaweza kupanga mipango ya maendeleo katika sekta mbalimbali.

Amesema kuwa takwimu hizo zitasaidia kuweka rasilimali ambazo zinatumika kukuza uchumi wa taifa ili kurahisisha upatikanaji wa huduma kwa jamii.



"Takwimu hizi zitasaidia kupatikana huduma za jamii kwa urahisi hivyo nawataka viongozi kutumia matokeo hayo katika ugawaji wa rasilimali kwa kuongeza maendeleo nchini," amesema Kitwana.

Sambamba na hayo ametoa wito kwa masheha na madiwani kuwa mstari wa mbele katika kufikisha taarifa hizo kwa jamii  ili kuisaidia serikali kutoa huduma sahihi  kwa wananchi.


Pia, Kitwana amewataka watendaji wa ngazi za Wadi na Shehia kuyatumia matokeo ya Sensa kuleta mabadiliko kwenye maeneo yao.

Kamisaa wa Sensa Zanzibar, Hamza Haji amesema kwa mujibu wa matokeo ya Sensa 2022, imeonesha kuwa Mkoa wa Mjini Magharibi una idadi kubwa ya wakazi ikilinganishwa na mikoa mingine ya Zanzibar.Hata hivyo ametoa pongezi kwa masheha  kufanikisha kazi hiyo kuanzia ngazi ya matayarisho hadi upatikanaji wa matokeo mazuri.



Kurasa

Translate

Popular Posts

Blog Archive

Tangazo!

JE UNAHITAJI KUBORESHA BLOG YAKO?

WEIGHT MANAGEMENT

WEIGHT MANAGEMENT

SIKILIZA NYIMBO MPYA

Watembeleaji

On Facebook

Tangazo Victoria!!

Date & Time

Weight Management



CLICK THIS IMAGE

Sikiliza Clouds Radio



Sikiliza Kwanza Jamii Radio

Total Pageviews

Fomu ya Anwani

Jina

Barua pepe *

Ujumbe *