WELCOME TORINTO HOT MEDIA BLOG | FOR MORE INFORMATION ABOUT OUR NEWS CONTACT US CELL: +255 756 188 180 | Email: josephlieme@gmail.com| KARIBU TORINTO HOT MEDIA BLOG | KWA MAELEZO ZAIDI KUHUSU HABARI ZETU WASILIANA NASI SIMU: +255 756 188 180 | Barua Pepe: josephlieme@gmail.com | DO YOU NEED TO DEVELOP YOUR BLOG CONTACT US CLICK HERE | JE UNAHITAJI KUBORESHA BLOG YAKO WASILIANA NASI BOFYA HAPA

Jumatano, 18 Januari 2017

 06:42      No comments
RC wa simiyu akizungumza pamoja na watendaji wa TBA Dar es salaam leo kabla kuanza kwa ziara hiyo
Na Joe Clanx Dar es Salaam.

 SOMA HABARI HII KISHA PICHA ZOTE ZA ZIARA TUMEKUWEKEA HAPO CHINI BAADA YA KUISOMA TAARIFA HII KARIBU


Jopo la viongozi wa mkoa wa Simiyu wakiongozwa na mkuu wa mkoa huo  Bw. Antoni Mtaka  hii leo wametembelea mradi wa majengo mapya ya hosteli za wanafunzi chuo kikuu cha Dar es Salaamu ili kujionea utendaji wa TBA juu ya garama za utekelezaji wa mradi pamoja na ufanisi mbalimbali unaotekelezwa na TBA ili kujionea unafuu wa garama za fedha katika utekelezaji wa miradi kiukandarasi hapa nchini.

Akizungumza na waandishi wa habari mkuu wa mkoa wa Simiyu amesema kuwa wamelazimika kufanya ziara ya kutembelea mradi wa ujenzi huo wa hosteli, unaotekelezwa na TBA ili kujifunza mambo mbalimbali yakiwemo unafuu wa kuwatumia wakandarasi wa hapa nchini ili kupunguza garama ambazo wakati mwingine  zinakuwa juu ikilinganishwa na ualisia wa majengo husika.

Pia ameeleza kilichopelekea wao kufanya ziara ni katika kutii agizo la Mh. Rais Dk. Jonh Magufuli ambapo aliwaagiza watembelee mradi huo wa hosteli uliojengwa na TBA ambao umetumia garama ya Bilioni kumi tu (10) hadi ujenzi kukamilika, huku ikiwa ni tofauti na garama walizoomba wao mkoa wa Simiyu kwa ajili ya ujenzi wa Hospitali ya Mkoa ambapo wao waliomba garama ya shilingi bilioni arobaini na sita (46)

Naye mkurugenzi mkuu wa TBA Elius Mwakalinga amesema kuwa baada ya kupokea taarifa iliyo mhusu meneja mkoa wa Simiyu kwa TBA kuweka makadirio ya ujenzi huo wa hospitali ya mkoa wa simiyu makubwa tofauti na ilivyodhaniawa hivyo ameamuw kumwamisha meneja huyu kutoka mkoa wa Simiyu na kurudi Makao makuu ya TBA ili kupisha timu ya uchunguzi itakayoenda kupitia upya michoro ya ramani pamoja na garama katika uandaaji wa ujenzi wa hospitali hiyo na kulinganisha na garama za wali alizokuwa ameziomba meneja huyo.
Mkurugenzi wa TBA Elius Mwakalinga akizungumza mbele ya mkuu wa mkoa wa simiyu kabla ya kuanza kwa ziara hiyo katiak ofisi ya makao makuu TBA.

Baadhi ya watendaji wa TBA na Viongozi wa Mkoa wa simiyu wakiendelea na kikao hivi leo kabla ya ziara.




Watendaji wa TBA  pamoja na viongozi kutoka mkoa simiyu wakielekea katika kukagua ujenzi wa hosteli za chuo kikuu cha Dar es salaam(UDSM)mara baada ya kuwasili eneo hilo

Baadhi ya mafundi wakiendelea na shughuli zao katika kuelekea kukamilika kwa ujenzi huo wa hosteli

Mkuu wa mkoa wa Simiyu Antoni Mtaka wakijadiliana jambo pamoja na mkuu wa kitengo cha mawasiliano cha wakala wa majengo TBA Edna Joseph mara baada ya kuwasili katika ujenzi huo

Kutoka kushoto ni mkuu wa mkoa wa Simiyu akikabidhiwa kofia na mkurugenzi wa TBA tayari kwa kuingia ndani ya ujenzi huo wa vyumba   katikati ni mkuu wa kitengo cha mawasiliano TBA



Hapa uongozi ulikuwa tayari kwa kwenda kukagua ujenzi huo pamoja na kujifunza mambo mbalimbali katika kutekelezwa kwa mradi huo


Mafundi wakiendelea na kazi katika kukamilisha chemba za maji machafu


Monekano wa majengo ya hosteli ya chuo kikuu cha DAR kama yanavyoonekana ambayo yamejengwa kwa garama nafuu na kutumia muda mfupi wa miezi tu hadi kufikia hapa






ukaguzi ukiendelea

Rc na uongozi wakikagua vyumba vya ndani katika hosteli


Mafundi umeme wakiendelea na kazi katika hosteli za UDSM

RC pamoja na uongozi wakikagua ujenzi wa bwalo la chakula UDSM


Hapa Rc wa Simiyu akifafanuliwa jambo na mkurugenzi wa TBA







Baadhi ya Mafundi na watendaji wakiendelea na majukumu yao





Viongozi wakikagua chumba cha hosteli ya wanafunzi UDSM



Picha zote na Joe Clanx



Asante kwa kuwa pamoja nasi mpendwa wetu

0 maoni:

Chapisha Maoni

Kurasa

Translate

Popular Posts

Blog Archive

Tangazo!

JE UNAHITAJI KUBORESHA BLOG YAKO?

WEIGHT MANAGEMENT

WEIGHT MANAGEMENT

SIKILIZA NYIMBO MPYA

Watembeleaji

On Facebook

Tangazo Victoria!!

Date & Time

Weight Management



CLICK THIS IMAGE

Sikiliza Clouds Radio



Sikiliza Kwanza Jamii Radio

Total Pageviews

Fomu ya Anwani

Jina

Barua pepe *

Ujumbe *