WELCOME TORINTO HOT MEDIA BLOG | FOR MORE INFORMATION ABOUT OUR NEWS CONTACT US CELL: +255 756 188 180 | Email: josephlieme@gmail.com| KARIBU TORINTO HOT MEDIA BLOG | KWA MAELEZO ZAIDI KUHUSU HABARI ZETU WASILIANA NASI SIMU: +255 756 188 180 | Barua Pepe: josephlieme@gmail.com | DO YOU NEED TO DEVELOP YOUR BLOG CONTACT US CLICK HERE | JE UNAHITAJI KUBORESHA BLOG YAKO WASILIANA NASI BOFYA HAPA

Jumatano, 18 Januari 2017

 06:31      No comments


SE1
Mwenyekiti wa Kitengo cha Nafaka na Mamalishe wa Soko la Kisutu jijini Dar es Salaam,Bw.  Mohamed Salum akielezea jambo kwa mwandishi wa habari kuhusu hali ya upatikanaji wa chakula katika Soko hilo leo jijini Dar es Salaam. Mohamed amesema kuwa chakula kinapatikana kwa wingi kutoka maeneo mbalimbali ya mikoa.
SE2
Picha ikionyesha baadhi ya nafaka zikiwa zinauzwa katika Soko la Kisutu jijini Dar es Salaam.
SE3 SE4
Mkazi wa jijini Dar es Salaam akinunua nafaka katika Soko la Kisutu jijini Dar es Salaam leo.
Picha na: Frank Shija – MAELEZO.
……………………………………………………………
Na: Frank Shija – MAELEZO.
HALI ya upatikanaji wa chakula nchini inaridhisha licha ya changamoto ya kuongezeka kwa bei ya bidhaa za chakula zitokanazo na nafaka.
Hayo yamebainishwa na Mwenyekiti wa Kitengo cha Nafaka na Mamalishe wa Soko la Kisutu jijini Dar es Salaam, Bwana Mohamed Salum katika mahojiano maalum na mwandishi wa habari hii leo jijini Dar es Salaam.
Mohamed amesema kuwa pamoja na kuwa Dar es Salaam inategemea chakula kutoka mikoani bado hali ya upatikanaji wake ni mkubwa na wa kuridhisha kama ambavyo imekuwa miaka ya nyuma.
“Chakula bado kinapatika kwa wingi japo changamoto iliyopo ni ongezeko la bei pekee kitu ambacho si kigeni duniani kote,” alisema Salum.
Alisema nia ajabu sana kusikia watu wanasema kuna baa la njaa wakati vyakula vinapatikana kwa wingi katika masoko yetu.
Aliongeza kuwa kungekuwa na tatizo la uhaba wa chakula basi hata uingizwaji wa chakula katika jiji la Dar es Salaam ungepungua kwani asilimia kubwa inategemea chakula kutoka mikoani, badala yake upatikanaji wa chakula umeendelea kuwa wa kuridhisha.
“Ndugu mwandishi ukitaka kujua kuwa hakuna uhaba wa chakula jaribu kutembelea maeneo ya Manzese Uzuri utajionea namna maroli matani kwa matani yanayoingiza nafaka kwenye mashine za kusaga na kukoboa.” Alisisitiza.

0 maoni:

Chapisha Maoni

Kurasa

Translate

Popular Posts

Blog Archive

Tangazo!

JE UNAHITAJI KUBORESHA BLOG YAKO?

WEIGHT MANAGEMENT

WEIGHT MANAGEMENT

SIKILIZA NYIMBO MPYA

Watembeleaji

On Facebook

Tangazo Victoria!!

Date & Time

Weight Management



CLICK THIS IMAGE

Sikiliza Clouds Radio



Sikiliza Kwanza Jamii Radio

Total Pageviews

Fomu ya Anwani

Jina

Barua pepe *

Ujumbe *