WELCOME TORINTO HOT MEDIA BLOG | FOR MORE INFORMATION ABOUT OUR NEWS CONTACT US CELL: +255 756 188 180 | Email: josephlieme@gmail.com| KARIBU TORINTO HOT MEDIA BLOG | KWA MAELEZO ZAIDI KUHUSU HABARI ZETU WASILIANA NASI SIMU: +255 756 188 180 | Barua Pepe: josephlieme@gmail.com | DO YOU NEED TO DEVELOP YOUR BLOG CONTACT US CLICK HERE | JE UNAHITAJI KUBORESHA BLOG YAKO WASILIANA NASI BOFYA HAPA

Jumatatu, 16 Oktoba 2023

 06:48      No comments

 Torintohot Blog.

 Na Jerome Mlaki wa Dar 


Dar es salaam,

Akizungumza katika uzinduzi wa maonesho hayo naibu waziri Kasekenya amesema maonesho hayo ni muhimu kwani yamewakutanusha wadau mbalimbali wa ujenzi kutoka ndani na nje ya nchi

Maonesho ya dar construction expo 2023 yamefunguliwa rasmi hii leo jijini Dar es salaam na naibu waziri wa ujenzi Godfray Kasekenya.

Kasekenya amesema kuwa sekta ya ujenzi hapa nchini imezidi kukua siku baada ya siku hivyo kupitia maonesho hayo watanzania wataweza kukutana na makampuni mbalimbali bora ya vifaa vya ujenzi kutoka hapa nchini na yale ya nje ya Tanzania.

"maonesho haya ni muhimu sana kwenye sekta ya ujenzi hivyo niwapongeze kampuni ya Dar expo kwa kuyaandaa"amesema Kasekenya


Awali akizungumza katika uzinduzi huo,muandaaji wa maonesho hayo Deogratius Kilawe amesema  Maonesho hayo yanatarajiwa kuwa ni ya siku Tatu kuanzia leo  Tarehe 11- 13 Oktoba 2023 ambapo yanafanyika katika Ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dae es salaam.

Amesema maonesho hayo ni jukwaa muhimu katika kuwakutanisha wadau wa sekta ya ujenzi.

Aidha katika hatua nyingine ameipongeza bodi ya wakandarasi hapa nchini kwa kusimamia ujenzi wa miundombinu mbalimbali yakiwemo madaraja na barabara zenye ubora hali iliyopelekea Taifa kuwa na Miundombinu bora.

0 maoni:

Chapisha Maoni

Kurasa

Translate

Popular Posts

Blog Archive

Tangazo!

JE UNAHITAJI KUBORESHA BLOG YAKO?

WEIGHT MANAGEMENT

WEIGHT MANAGEMENT

SIKILIZA NYIMBO MPYA

Watembeleaji

On Facebook

Tangazo Victoria!!

Date & Time

Weight Management



CLICK THIS IMAGE

Sikiliza Clouds Radio



Sikiliza Kwanza Jamii Radio

Total Pageviews

Fomu ya Anwani

Jina

Barua pepe *

Ujumbe *