WELCOME TORINTO HOT MEDIA BLOG | FOR MORE INFORMATION ABOUT OUR NEWS CONTACT US CELL: +255 756 188 180 | Email: josephlieme@gmail.com| KARIBU TORINTO HOT MEDIA BLOG | KWA MAELEZO ZAIDI KUHUSU HABARI ZETU WASILIANA NASI SIMU: +255 756 188 180 | Barua Pepe: josephlieme@gmail.com | DO YOU NEED TO DEVELOP YOUR BLOG CONTACT US CLICK HERE | JE UNAHITAJI KUBORESHA BLOG YAKO WASILIANA NASI BOFYA HAPA

Jumatano, 4 Oktoba 2023

 13:10      No comments



Na Jerome Mlaki wa Dar

Mamlaka ya huduma za nishati na maji nchini (EWURA) usiku wa kuamkia leo, imetangaza bei mpya za mafuta zitakazoanza kufanya kazi kuanzia Jumatano hii, Oktoba 04, 2023 ambapo katika bei hizo inaonesha mafuta ya Dizeli yamepanda zaidi ukilinganisha na aina nyingine za mafuta 

Taarifa kwa umma iliyotolewa na mamlaka hiyo inaonesha kuwa mafuta ya Dizeli sasa yatapatikana kwa Tsh.3520/- kwa lita wakati Petroli na mafuta ya taa yatakuwa yanauzwa kwa Tsh.3353/- na Tsh.3016/-

Imeelezwa sababu ya kupanda kwa bei hizo kuwa ni kupanda kwa gharama za mafuta katika soko la Dunia hadi kufikia asilimia 4.21 na gharama za uagizaji wa mafuta hadi kufikia asilimia 17 kwa Petrol, asilimia 62 kwa Dizeli na asilimia 4 kwa mafuta ya taa, lakini pia sababu nyingine iliyotajwa kupelekea kupaa kwa bei hizo ni uamuzi wa wazalishaji wakubwa wa mafuta Duniani (OPEC+) kupunguza uzalishaji na vikwazo vya kiuchumi ambavyo nchi ya Urusi imewekewa na mataifa ya magharibi

Aidha katika taarifa hiyo ya EWURA iliyosainiwa na Mkurugennzi Mkuu wake Dkt.James Mwainyekule imewakumbusha wafanyabiashara wa bidhaa za mafuta kwa jumla na rejareja sambamba na jamii yote kuzingatia bei za kikomo zilizowekwa 

Katika bei hizo ambazo zonapaswa kuchapishwa kwenye mabango yanayoonekana bayana katika vituo vyote vya mafuta nchini zinaonesha kuwa bei za rejareja za mafuta ya Petrol kwa mikoa ya Dar es Salaam, Tanga na Mtwara kuwa ni Tsh.3281/-, Tsh.3287/- na Tsh.3283/-, Dizeni ni Tsh.3448/-, Tsh.3494/- na Tsh.3590/- na mafuta ya taa ni Tsh.2943/-, Tsh.2989/- na Tsh.3016/- kwa lita

0 maoni:

Chapisha Maoni

Kurasa

Translate

Popular Posts

Blog Archive

Tangazo!

JE UNAHITAJI KUBORESHA BLOG YAKO?

WEIGHT MANAGEMENT

WEIGHT MANAGEMENT

SIKILIZA NYIMBO MPYA

Watembeleaji

On Facebook

Tangazo Victoria!!

Date & Time

Weight Management



CLICK THIS IMAGE

Sikiliza Clouds Radio



Sikiliza Kwanza Jamii Radio

Total Pageviews

Fomu ya Anwani

Jina

Barua pepe *

Ujumbe *