WELCOME TORINTO HOT MEDIA BLOG | FOR MORE INFORMATION ABOUT OUR NEWS CONTACT US CELL: +255 756 188 180 | Email: josephlieme@gmail.com| KARIBU TORINTO HOT MEDIA BLOG | KWA MAELEZO ZAIDI KUHUSU HABARI ZETU WASILIANA NASI SIMU: +255 756 188 180 | Barua Pepe: josephlieme@gmail.com | DO YOU NEED TO DEVELOP YOUR BLOG CONTACT US CLICK HERE | JE UNAHITAJI KUBORESHA BLOG YAKO WASILIANA NASI BOFYA HAPA

Jumatano, 30 Mei 2018

 04:42      No comments





Na Jerome Mlaki

MANISPAA ya Ilala imetakiwa kuanzisha klabu za mazingira katika shule zake za msingi za manispaa hiyo ili wanafunzi wafundishwe umuhimu wa utunzaji mazingira. 

Ushauri huo umetolewa Dar es Salaam jana na Ofisa Tawala wa Wilaya ya Ilala Jabiri Makame wakati wa kampeni ya  upandaji miti shule msingi Yongwe iliyopo Chanika ILALA.

"Naomba Idara ya Mazingira manispaa ya Ilala muunde vilabu vya mazingira katika shule zenu za msingi ili wanafunzi wafundishwe umuhimu wa utunzaji wa mazingira"alisema Makame. 

Makame alisema suala la utunzaji wa mazingira ni letu sote hivyo inatakiwa tuweke mikakati mbalimbali jinsi ya uendelezaji na utunzaji wa mazingara. 

Alisema ikiwekwa mikakati endelevu ya kuanzisha vilabu mashuleni wanafunzi wakafahamu jinsi  utunzaji mazingira serikali itakuwa imefaidika jamii nzima itapata elimu hiyo. 


Amewapongeza Benki ya Standard Chartered Tanzania kwa juhudi zao kwa kuwekeza shule za msingi hasa upande wa mazingira na kuwataka wadau wengine Kushirikia na serikali. 

    Alisema utunzaji wa mazingira unafaida nyingi nchi yetu inaepuka jangwa,faida nyingine miti inaleta kivuli na miti mingine ya matunda. 

Kwa upande wake Ofisa Elimu Msingi Ilala Elzabeth, thomas alisema Standard Chartered wameanza kampeni ya kusaidia shule za Msingi Ilala toka mwaka 2014  mpaka sasa wameweza kupanda miti 3300.


Thomas alisema kuanzia mwaka 2014 hadi sasa wamekuwa wakishirikiana katika utunzaji wa mazingira  katika shule mbalimbali. 

Alisema awali kabla kupanda miti SHULE ya Yongwe kampeni hiyo ilianzia shule ya msingi Majani ya Chai, Pugu Kajiungeni, Buyuni, Kigogo Freshi, Viwege na Uhuru Mchanganyiko. 

Kwa upande wake Ofisa wa Benki hiyo  Isema Bilali alisema benki hiyo ilianza shughuli zake nchini mwaka 1917  na baadae mwaka 1993 mara baada kuundwa kwa azimio la Arusha ambapo kwa sasa inashirikiana pia na serikali katika shughuli za kijamii. 

Bilali alisema  upandaji miti una faida nyingi ikiwemo kutuwezesha kupata mvua,ujenzi,inatupa chakula inazuia mmomonyoko wa udongo. 

0 maoni:

Chapisha Maoni

Kurasa

Translate

Popular Posts

Blog Archive

Tangazo!

JE UNAHITAJI KUBORESHA BLOG YAKO?

WEIGHT MANAGEMENT

WEIGHT MANAGEMENT

SIKILIZA NYIMBO MPYA

Watembeleaji

On Facebook

Tangazo Victoria!!

Date & Time

Weight Management



CLICK THIS IMAGE

Sikiliza Clouds Radio



Sikiliza Kwanza Jamii Radio

Total Pageviews

Fomu ya Anwani

Jina

Barua pepe *

Ujumbe *