WELCOME TORINTO HOT MEDIA BLOG | FOR MORE INFORMATION ABOUT OUR NEWS CONTACT US CELL: +255 756 188 180 | Email: josephlieme@gmail.com| KARIBU TORINTO HOT MEDIA BLOG | KWA MAELEZO ZAIDI KUHUSU HABARI ZETU WASILIANA NASI SIMU: +255 756 188 180 | Barua Pepe: josephlieme@gmail.com | DO YOU NEED TO DEVELOP YOUR BLOG CONTACT US CLICK HERE | JE UNAHITAJI KUBORESHA BLOG YAKO WASILIANA NASI BOFYA HAPA

Jumanne, 10 Oktoba 2017

 04:35      No comments


 TAGS

Serikali yatakiwa kurekebisha Sheria ya adhabu ya kifo

                          Na Mwandishi wetu-Utouh News


Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imetakiwa kurekebisha Sheria ya kanuni ya adhabu na Sheria ya ugaidi yenye kutoa adhabu ya kifo kwa makosa ya mauaji ,uhaini na ugaidi.

Hayo yamejiri jijini Dar es salaam wakati wa maadhimisho ya miaka 15 ya siku ya kupinga adhabu ya kifo duniani yenye kauli mbiu isemayo ''umaskini na haki ni mchanganyiko hatari''.

Akizungumza na wanahabari Mratibu wa Dawati la Katiba wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu ANNA HENGA amesema kuwa wanapinga adhabu ya kifo kwa sababu ni adhabu ya kibaguzi na kikatili inayotweza utu wa binadamu.

"tunapenda kuweka wazi kwamba hatukubaliani kwa namna yeyote na vitendo vya mauaji na tusingependa kuona muuwaji anauwawa baada ya kuua,kufanya hivyo ni kuhalalisha kifo",alisema Henga.

Aidha amempongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt JOHN MAGUFULI kwa kuweka wazi msimamo wake wa kutokuunga mkono adhabu ya kifo kwani ni adhabu ya kinyama na isiyomstahili binadamu yeyote Yule.

Takwimu zinaonyesha mpaka kufikia mwaka 2015 kulikuwa na jumla ya watu 472 waliokuwa wamehukumiwa kunyongwa ambao kati yao 452 ni wanaume na 20 ni wanawake.

0 maoni:

Chapisha Maoni

Kurasa

Translate

Popular Posts

Blog Archive

Tangazo!

JE UNAHITAJI KUBORESHA BLOG YAKO?

WEIGHT MANAGEMENT

WEIGHT MANAGEMENT

SIKILIZA NYIMBO MPYA

Watembeleaji

On Facebook

Tangazo Victoria!!

Date & Time

Weight Management



CLICK THIS IMAGE

Sikiliza Clouds Radio



Sikiliza Kwanza Jamii Radio

Total Pageviews

Fomu ya Anwani

Jina

Barua pepe *

Ujumbe *