WELCOME TORINTO HOT MEDIA BLOG | FOR MORE INFORMATION ABOUT OUR NEWS CONTACT US CELL: +255 756 188 180 | Email: josephlieme@gmail.com| KARIBU TORINTO HOT MEDIA BLOG | KWA MAELEZO ZAIDI KUHUSU HABARI ZETU WASILIANA NASI SIMU: +255 756 188 180 | Barua Pepe: josephlieme@gmail.com | DO YOU NEED TO DEVELOP YOUR BLOG CONTACT US CLICK HERE | JE UNAHITAJI KUBORESHA BLOG YAKO WASILIANA NASI BOFYA HAPA

Jumanne, 10 Oktoba 2017

 04:34      No comments


 TAGS
Mwanza. Mkuu wa Shule ya Sekondari Migukulama iliyopo Halmasahauri ya Buchosa wilayani Sengerema, Benerdicto Lweikiza (45) amejinyonga hadi kufa akiwa chumbani kwake.

Taarifa za kujinyonga kwa mwalimu huyo zilianza kusambaa wilayani Sengerema na kuthibitishwa na Mkurugenzi Mtendaji wa wa Halmashauri ya Buchosa, Crispin Luanda.

“Ni kweli mwalimu huyo amejinyonga alikuwa mkuu wa Shule ya Sekondari Migukulama na amefikia uamuzi huo majira ya saa tisa mchana wa leo (jana) nyumbani kwake Mtaa wa Kilabela mjini Sengerema,” alisema Luanda.

Mmoja wa wanafamilia wa mwalimu huyo, Martin Kalemera alisema kuwa wao kama familia wanashangazwa na suala hilo na hawaamini kilichotokea ikiwa ni miaka mitano imepita tangu mke wake afariki dunia.

Mkuu wa Wilaya ya Sengerema, Emmanuel Kipole alithibitisha kupata taarifa ya kifo cha mwalimu huyo na kusema kuwa hajafahamu chanzo cha kufikia hatua ya kujinyonga na kamba chumbani kwake.

Alisema vyombo vya dola vinafuatilia kwa kina ili kubaini sababu.

Tukio hilo lilitokea saa chache baada ya gari aina ya Toyota Hiace kutumbukia ndani ya Ziwa Victoria na kuua zaidi ya watu 12 katika eneo la Kivuko cha Kigogo wilayani Misungwi.

0 maoni:

Chapisha Maoni

Kurasa

Translate

Popular Posts

Blog Archive

Tangazo!

JE UNAHITAJI KUBORESHA BLOG YAKO?

WEIGHT MANAGEMENT

WEIGHT MANAGEMENT

SIKILIZA NYIMBO MPYA

Watembeleaji

On Facebook

Tangazo Victoria!!

Date & Time

Weight Management



CLICK THIS IMAGE

Sikiliza Clouds Radio



Sikiliza Kwanza Jamii Radio

Total Pageviews

Fomu ya Anwani

Jina

Barua pepe *

Ujumbe *