WELCOME TORINTO HOT MEDIA BLOG | FOR MORE INFORMATION ABOUT OUR NEWS CONTACT US CELL: +255 756 188 180 | Email: josephlieme@gmail.com| KARIBU TORINTO HOT MEDIA BLOG | KWA MAELEZO ZAIDI KUHUSU HABARI ZETU WASILIANA NASI SIMU: +255 756 188 180 | Barua Pepe: josephlieme@gmail.com | DO YOU NEED TO DEVELOP YOUR BLOG CONTACT US CLICK HERE | JE UNAHITAJI KUBORESHA BLOG YAKO WASILIANA NASI BOFYA HAPA

Jumanne, 14 Februari 2017

 04:19      No comments

Displaying DSC05685.JPG

TAARIFA KWA UMMA

1.0. UTANGULIZI

Ndugu Wanahabari na Watanzania wote, Kheri ya mwaka mpya 2017!

Baada ya mapumziko ya sikukuu za Krisimasi pamoja na mwaka mpya, tumewaita leo

hapa, lengo kuu likiwa ni kuwasiliana na umma kupitia vyombo vya habari kuhusu

masuala kadhaa yanayohusu mchakato wa katiba mpya pamoja na maendeleo ya

Tanzania katika ujumla wake. Tumeendelea kufuatilia maendeleo ya mchakato wa

katiba kwa umakini mkubwa, usiku na mchana ili kuhakikisha wananchi wanapata

taarifa muhimu na sahihi kuhusu mchakato wa katiba mpya. Katika kufuatilia kwetu

huku, tumebaini pia zipo changamoto zingine za kiutendaji kwa baadhi ya viongozi

waandamizi wa serikali. Aidha, tumeshangazwa sana na kitendo cha Jeshi la Polisi

kuanza kutekeleza agizo la kung’oa matairi kwenye vyombo vya moto vinavyokamatwa

vimepita kwenye barabara ya mabasi ya mwendo kasi. Mbaya, zaidi, agizo hilo lilitolewa

na Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Magufuli, na Jeshi la Polisi kuanza kulifanyia kazi


Displaying DSC05701.JPG

bila kujali kuwa lipo kinyume na katiba na sheria na kwamba linaweza kusababisha

usumbufu mkubwa kuliko tatizo lenyewe.

Itakumbukwa pia kuwa vitendo vingine kadhaa vimeendelea kufifisha utawala wa sheria

nchini. Kwanza, kamata kamata ya raia na viongozi wanaoonekana kuwa na mwelekeo

wa kukosoa serikali au watawala binafsi. Ingawa JUKATA hatujawahi kutetea

wanaokashifu au kutukana viongozi, uvumilivu na staha kwa wakosoaji wa kawaida

unahitajika sana. Pili, kumekuwa na tabia ya baadhi ya viongozi wa serikali kutaja

majina ya watu na kuwahusisha waziwazi na uhalifu kabla vyombo husika

havijakamilisha uchunguzi ni kinyume cha misingi ya utawala bora na ibara ya 13 (6)

(d) ya Katiba ya Tanzania. Aidha vitendo vya polisi kuadhibu madereva kwa baadhi ya

makosa ya usalama barabarani ambayo hayajatendwa kunazidi kuwatia unyonge

watanzania kiasi cha kujiona kama watumwa ndani ya nchi yao wenyewe kinyume na

uhuru unaoelezwa katika ibara ya 15 (1). Aidha, marufuku kwa mikutano ya kisiasa

inayoendelea nchini siyo tu inabana haki na uhuru wa kujumuika, kutoa maoni na

kueleza fikra zake kwa mujibu wa ibara ya 18 na 20 (1) za Katiba ya Tanzania bali pia

imeua hamasa na ari ya wananchi iliyokuwepo wakati wa uongozi wa awamu ya nne.

Kwa vitendo kama hivi na vingine vingi, hoja ya kuwa na katiba itakayowadhibiti

viongozi wenye kudhani neno lao ndio kauli ya mwisho ama sheria ya nchi inapata

msukumo mkubwa.

Displaying DSC05681.JPG

2.0. MKANGANYIKO WA KAULI ZA SERIKALI KUHUSU MCHAKATO WA

KATIBA MPYA

Ndugu wanahabari na Watanzania wote,

JUKATA tumeendelea kupokea malalamiko kutoka kwa wananchi wakiomba ufafanuzi

wa kauli kinzani juu ya mchakato wa katiba mpya kutoka kwa viongozi wa serikali.

Wananchi wanahoji ipi kauli ya serikali kuhusu mwelekeo wa katiba mpya?. Kwa nyakati

tofauti, Mhe. Rais Dkt. John Pombe Magufuli ametoa kauli za kuvunja moyo ama kuleta

faraja juu ya mwelekeo wa katiba mpya. Hivyo, wananchi wanahitaji ufafanuzi na

msimamo wa serikali ya awamu ya tano juu ya mchakato wa katiba mpya. Kwa mfano,

tarehe 23 Juni 2016, Rais alipokuwa akipokea taarifa ya uchaguzi mkuu wa Oktoba

2015 kutoka kwa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) alipongeza jitihada zilizofanywa na

serikali ya awamu ya nne kwenye mchakato wa katiba mpya. Kwa maneno yake,

aliahidi kuhakikisha Tanzania inapata katiba mpya katika kipindi chake cha uongozi.

Lakini pia, kwa mshangao mkubwa na kinyume na maneno yake mwenyewe, tarehe 4

3

Novemba 2016, Mhe. Rais John Pombe Magufuli alipokuwa akiongea na waandishi wa

habari Ikulu, Dar es Salaam, alisema katiba mpya sio kipaumbele cha serikali yake na

kwamba kwenye kampeni zake hakusema chochote kuhusu katiba mpya.

Kwa kauli hii, na ile ya awali wananchi wengi wamebaki njia panda. Watanzania

wanapenda kuelewa nini msimamo wa serikiali ya awamu ya tano kuhusu mchakato wa

katiba mpya. Ifahamike pia, baadhi ya watanzania ambao walikuwa mstari wa mbele

kudai katiba mpya ya wananchi, kwa nyakati mbalimbali wameendelea kupata uteuzi

ama wa kushika nyadhifa ndani ya Chama Tawala au Serikalini. Wananchi wanahoji je

uteuzi wa namna hii unaashiria nini kuhusu mchakato wa katiba Mpya? JUKATA

tunapenda kumsihi Mhe. Rais ajizuie kutoa kauli ambazo zinawayumbisha na

kuwachanganya wananchi anaowaongoza. Atoe kauli moja kuhusu katiba mpya ambayo

itafuatwa na vyombo vya serikali kama ile ya kung’oa matairi kwenye vyombo vya moto

ilivyoanza kutekelezwa na Jeshi la Polisi.

3.0. KUKOSEKANA KWA TAARIFA RASMI YA SERIKALI KUHUSU

HATMA YA MCHAKATO WA KATIBA

Ndugu wanahabari, achilia mbali uwepo wa kauli kadhaa kuhusu mchakato wa katiba

kutoka kwa viongozi wa serikali, sasa ni zaidi ya mwaka mmoja tangu serikali ya awamu

ya tano iingie madarakani na hakuna taarifa rasmi ya serikali kuhusu mchakato wa

katiba. Kwa kipindi chote hiki, serikali haijaweza kuweka bayana dira na mwelekeo wa

mchakato wa katiba mpya. Yalikuwa ni mategemeo ya watanzania wengi kwamba

serikali ya awamu ya tano chini ya Mhe. Rais Magufuli ingeweza kutoa mwelekeo rasmi

wa mchakato wa katiba katika kipindi cha mwaka mmoja. Lakini serikali imeendelea

kukaa kimya bila kutoa kutoa taarifa rasmi ya serikali. Kukosekana kwa taarifa rasmi

kumeendelea kusababisha wananchi kukata tamaa ya kupata katiba mpya ambayo

ingeweza kutatua changamoto zao kwa kiwango kikubwa. Kama serikali ilivyo na

mipango mingi, ni muda muafaka serikali ikaleta mpango mkakati wa kumalizia

mchakato wa katiba ili wananchi wajiandae vema kushiriki kwenye hatua zitakazofuata

wakiwa na taarifa za kutosha.

4.0. HOJA YA MAREKEBISHO YA SHERIA ZINAZOSIMAMIA

MCHAKATO HAIEPUKIKI

Kama tulivyosema siku za nyuma na kwenye kitabu cha ‘Mwelekeo wa Katiba Mpya

Tanzania’ ipo haja ya kurekebisha sheria zinazosimamia mchakato wa katiba. Tangu

kuanza kwake, mchakato huu wa Katiba umeongozwa na sheria mbili kwa vipindi

4

tofauti. Awali, mchakato ulikuwa ukiongozwa na sheria ya Mabadiliko ya Katiba Na. 8 ya

mwaka 2011 (pamoja na marekebisho yake) na baada ya kupitishwa kwa Katiba

Inayopendekezwa, Sheria ya Kura ya Maoni ya mwaka 2013 ikaanza kutumika pia. Hata

hivyo, kwa sasa sheria hizi haziwezi kutumika tena kuongoza mchakato bila kufanyiwa

marekebisho kwa sababu za msingi kuu mbili ambazo ni kupitwa na wakati pamoja na

utata wa sheria hizo hasa sheria ya Kura ya Maoni. Kwa ukweli huu, serikali kupitia

Wizara husika kabla ya bunge la bajeti ipeleke muswada wa kurekebisha sheria hizi ili

kuzipa uhai na ziendelee kuongoza mchakato. Mabadiliko ya sheria hizi hayakwepeki

hata kidogo. Serikali pamoja na bunge ni lazima watekeleze jambo hili haraka

iwezekanavyo.

5.0. MUDA WA KATIBA MPYA NI SASA !

Ndugu wanahabari, tunatambua kuwa mchakato wa katiba mpya ulijisitisha wenyewe ili

kupisha Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015. Kwa uzoefu wetu kutokana na michakato ya

ujenzi wa katiba ndani na nje ya Tanzania, muda muafaka wa kukamilisha mchakato

huu muhimu ni sasa yaani 2017 hadi 2018. Kipindi hiki kisipotumika kukamilisha

mchakato wa katiba, ipo hatari katiba mpya kupatikana baada ya 2020. Hii ni kwa

sababu mwaka 2019 ni mwaka wa uchaguzi wa serikali za mitaa. Na baada ya uchaguzi

wa serikali za mitaa, joto la uchaguzi mkuu wa 2020 litakuwa juu. Kwa mantiki hiyo,

itakuwa ni hatari kuendelea na mchakato wa katiba katika mazingira ambayo wananchi

watakuwa kwenye maandalizi ya uchaguzi. Mchakato utaingia kwenye mkwamo kama

ule wa mwaka 2015 wakati wa Uchaguzi Mkuu. Tunaitaka serikali ya awamu ya tano

ivunje ukimya, iueleze umma wa watanzania mwelekeo wa kupata katiba mpya ni upi,

na lini mchakato utarejea tena. Ni vyema kabla ya kumalizika kwa robo ya kwanza ya

mwaka 2017 serikali ikaweka bayana jambo hili. Katiba mpya ni sasa. Mwaka 2017

unaweza kutumika kurekebisha kasoro kadhaa za kimaudhui katika Katiba

Inayopendekezwa na mwaka 2018 kura ya maoni ikafanyika kupitisha katiba mpya.

Muda ni huu, katiba ni sasa.

6.0. MAANDALIZI YA MKUTANO MKUU WA KITAIFA WA KATIBA

Ndugu wanahabari,

Kama tulivyosema mwaka jana wakati wa uzinduzi wa kitabu cha Mwelekeo wa

Katiba Mpya Tanzania, njia mojawapo inayoweza kutumika kukamilisha mchakato wa

katiba kwa hali ilivyo sasa ni Mkutano Mkuu wa Kitaifa wa Katiba. Hivyo basi, JUKATA

linapenda kuwajulisha watanzania kuwa, linaratibu maandalizi ya Mkutano Mkuu wa

Kitaifa wa Katiba utakaofanyika kuanzia tarehe 2 hadi 3 mwezi Machi, 2017 kwenye

5

Hoteli ya Landmark Jijini Dar es Salaam. Katika mkutano huo, wadau watakaopata fursa

ya kushiriki ni serikali, asasi za kiraia, taasisi za kidini, wabunge, vyama vya siasa na

makundi mbalimbali ya kijamii ambao watajadili kwa kina Mchakato wa Katiba

Tanzania: tulipotoka, tulipo, uzoefu kutoka nchi zingine pamoja na tuendako kwenye

mchakato wa kupata katiba mpya. Wasomi wabobevu wa masuala ya michakato ya

kidemokrasia kutoka ndani na nje ya nchi watafanya uchambuzi wa kina tangu kuanza

kwa mchakato wa katiba na kushauri mwelekeo mpya kutoka hapa tulipo. Hii itasaidia

kubaini changamoto tulizopitia na kuzifanyia kazi ili tufikie mwisho wa mchakato wa

katiba mpya. Ni rai yetu kwamba vyombo vya habari viwajulishe wananchi juu ya

mkutano huu muhimu ili waweze kufuatilia taarifa za mkutano huu kwa kushiriki au

kupitia vyombo vya habari muda utakapofika.

7.0. UZINDUZI WA FILAMU KUHUSU MCHAKATO WA KATIBA

TANZANIA

JUKATA inapenda kuufahamisha umma wa watanzania kuwa, baada ya JUKATA

kushiriki kikamilifu kwenye mchakato wa kuandika katiba mpya, hivi karibuni itazindua

filamu fupi ya dakika ishirini yenye lengo la kuonyesha matukio muhimu tangu

mchakato wa katiba ulipoanza. Katika filamu hiyo, JUKATA imeweza kuwahoji watalaam

mbalimbali walioshiriki kwenye mchakato wa katiba katika hatua mbalimbali. Pia,

JUKATA imeweza kupata maoni kutoka kwa wananchi wakielezea ushiriki wao kwenye

mchakato katika hatua zote. Aidha, katika filamu hiyo, wananchi kwa maoni yao

wenyewe wamebainisha namna bora ya kukamilisha mchakato wa katiba ili kupata

katiba mpya. JUKATA inatoa wito kwa waandishi wa habari na vyombo vya habari

nchini kutumia filamu hii kuendelea kuhabarisha umma juu ya haja ya wananchi

kuendelea kushiriki kwenye mchakato wa katiba mpya bila kujali changamoto

zinazojitokeza.

8.0. SERIKALI ITENGE BAJETI 2017/2018

Wadau wote, wanapaswa kurudi kwenye hamasa iliyokuwepo wakati wa Mchakato wa

kuandika katiba mpya awamu ya kwanza mwaka 2011-2014. Wakati na baada uchaguzi

mkuu wa 2015, hamasa hii imeendelea kushuka. Ni muhimu kwa wadau wote kutumia

muda huu kuanza kumalizia awamu ya pili ya mchakato wa kuandika katiba mpya kabla

hamasa hii muhimu ya wananchi wa Tanzania haijatoweka kabisa. Wadau wote

watambue kuwa, zaidi ya bilioni 100 zilitumika kwenye mchakato wa katiba hasa katika

hatua ya uundaji na uendeshaji wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba (TMK) na uundaji na

uendeshaji wa Bunge Maalum la Katiba (BMK). Fedha hizi zilitokana na kodi za

6

watanzania masikini. Hivyo, kuuacha mchakato wa katiba kama ulivyo sasa ni matumizi

mabaya ya fedha za umma na ni sawa na wizi au utapeli wa kawaida ambao serikali

imewafanyia wananchi wake. Kwa upande mwingine, Serikali kama mdau muhimu

kwenye mchakato wa katiba isiogope gharama ya kukamilisha mchakato wa katiba.

Hatua zilizobaki zinahitaji kwa kiwango kikubwa utashi wa kisiasa kuliko rasilimali fedha.

Ni wito wetu kwa serikali kwamba, katika bajeti ya fedha 2017/2018 itengwe fedha kwa

ajili ya kukamilisha mchakato huu.

9.0. HITIMISHO

JUKATA tunaamini kiongozi bora ni yule atakayekidhi matakwa ya Katiba ya wananchi.

Aidha, JUKATA tunaamini pia kuwa Katiba iliyopo ndiyo muongozo mkuu wa utawala wa

Nchi na haipaswi kusiginwa kwa namna yoyote ile. Kwa vile wananchi bado wana

hamasa ya kupata katiba mpya, ni muhimu kwa viongozi kuhakikisha katiba mpya

inapatikana kwa vile pia Katiba ndio waraka unaowawezesha wananchi kujitambua

kama taifa. Pia, katiba ni waraka wa kiutawala unaoeleza bayana mgawanyo na

majukumu ya vyombo mbalimbali vya dola katika nchi, hivyo katiba ndio waraka mama

wa kisheria na kisiasa unaoongoza shughuli zote za nchi na ni chimbuko la sheria zote

katika nchi. Bila katiba shughuli za serikali na za wananchi haziwezi kufanyika kwa

ufanisi. Ni wito wetu kwa serikali kukamilisha mchakato wa Katiba Mpya ifikapo mwaka

2018 kwani baada ya hapo siasa za kuelekea ikulu na majimboni zitafanya uwezekano

wa Katiba Kuandikika kuwa mdogo. Katiba mpya ni sasa !

Imetolewa na JUKATA na kusainiwa na;

Deus M.Kibamba

Mwenyekiti wa Bodi

0 maoni:

Chapisha Maoni

Kurasa

Translate

Popular Posts

Blog Archive

Tangazo!

JE UNAHITAJI KUBORESHA BLOG YAKO?

WEIGHT MANAGEMENT

WEIGHT MANAGEMENT

SIKILIZA NYIMBO MPYA

Watembeleaji

On Facebook

Tangazo Victoria!!

Date & Time

Weight Management



CLICK THIS IMAGE

Sikiliza Clouds Radio



Sikiliza Kwanza Jamii Radio

Total Pageviews

Fomu ya Anwani

Jina

Barua pepe *

Ujumbe *