Mkuu wa Itifaki mstaafu Balozi Cisco Mtiro anatarajiwa kuzikwa kesho baada ya kufariki hospitali ya Aga Khan jijini Dar es salaam alikokuwa amelazwa kwa matibabu, kwa mujibu wa msemaji wa familia, Bw. Shaaban Kessy Mtambo
Msemaji wa familia Shaaban Mtambo amesema kwamba mazishi ya mwanadiplomasia huyo yamepangwa kufanyika siku ya Jumatano saa saba adhuhuri katika makaburi ya Kisutu jijini Dar es salaam.
Alisema mke wa marehemu anatarajia kuingia leo mchana kutokea Bangui, AfrikaKusini na watoto wake walioko Marekani ambao wanategemewa kuwasili leo usiku, kwaajiri ya mazishi.
Amesema mwili wa marehemu unatarajiwa kuwasili nyumbani kwa marehemu saa tano asubuhi siku hiyo ya Jumatano ambapo utafanyiwa kisomo na kuswaliwa kabla ya kuelekea makaburini kwa mazishi.
Msiba upo nyumbani kwa marehemu mikocheni B jijini Dar es salaam ambako ndugu, jamaa marafiki, majirani na waliofanya kazi na marehemu wamekuwa wakimiminika kutoa mkono wa pole kutwa nzima ya leo.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli ametuma salamu za rambirambi kufuatia msiba huu.
0 maoni:
Chapisha Maoni