WELCOME TORINTO HOT MEDIA BLOG | FOR MORE INFORMATION ABOUT OUR NEWS CONTACT US CELL: +255 756 188 180 | Email: josephlieme@gmail.com| KARIBU TORINTO HOT MEDIA BLOG | KWA MAELEZO ZAIDI KUHUSU HABARI ZETU WASILIANA NASI SIMU: +255 756 188 180 | Barua Pepe: josephlieme@gmail.com | DO YOU NEED TO DEVELOP YOUR BLOG CONTACT US CLICK HERE | JE UNAHITAJI KUBORESHA BLOG YAKO WASILIANA NASI BOFYA HAPA

Jumanne, 25 Julai 2023

 03:32      No comments

Torinto Hot Media Blog.




Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe Albert Chalamila leo Julai 22, 2023 ameongoza wadau wa TCC na Chama cha washereheshaji Tanzania na wakazi wa Kigamboni kufanya usafi fukwe ya pweza Wilaya ya Kigamboni ikiwa ni Kampeni ya safisha, Hifadhi Bahari.


Akiongea wakati wa zoezi hilo RC Chalamila ametoa rai kwa wadau wengine kuunga mkono juhudi za safisha, Hifadhi Bahari na kufanya usafi katika maeneo mengine ya Jiji hilo ambapo amekaribisha wadau wenye dhamira ya kuwekeza katika taka kuja kuwekeza.


Aidha Mhe Chalamila ametoa taarifa ya kufanyika kwa Mkutano Mkubwa wa wakuu wa nchi za Afrika kuhusu Rasirimali watu hivyo Jamii na wakazi wote kuendelea kufanya usafi na kuliweka Jiji safi ili kuleta taswira nzuri ya nchi yetu.


Vilevile kwa upande wa Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni Mhe Halima Bulembo amesema Wilaya hiyo ni moja ya Wilaya za Mkoa wa Dar es Salaam yenye fukwe nyingi ambazo ni muhimu katika sekta ya utalii wa fukwe hivyo Kampeni ya safisha Hifadhi Bahari ni muhimu kwa mstakabali wa kuwa na fukwe bora na zinazovutia.


Mwisho Mhe RC amekabidhiwa vifaa mbalimbali vya usafi kama mifagio, pipa la kuhifadhia taka na life Jacket

0 maoni:

Chapisha Maoni

Kurasa

Translate

Popular Posts

Blog Archive

Tangazo!

JE UNAHITAJI KUBORESHA BLOG YAKO?

WEIGHT MANAGEMENT

WEIGHT MANAGEMENT

SIKILIZA NYIMBO MPYA

Watembeleaji

On Facebook

Tangazo Victoria!!

Date & Time

Weight Management



CLICK THIS IMAGE

Sikiliza Clouds Radio



Sikiliza Kwanza Jamii Radio

Total Pageviews

Fomu ya Anwani

Jina

Barua pepe *

Ujumbe *