WELCOME TORINTO HOT MEDIA BLOG | FOR MORE INFORMATION ABOUT OUR NEWS CONTACT US CELL: +255 756 188 180 | Email: josephlieme@gmail.com| KARIBU TORINTO HOT MEDIA BLOG | KWA MAELEZO ZAIDI KUHUSU HABARI ZETU WASILIANA NASI SIMU: +255 756 188 180 | Barua Pepe: josephlieme@gmail.com | DO YOU NEED TO DEVELOP YOUR BLOG CONTACT US CLICK HERE | JE UNAHITAJI KUBORESHA BLOG YAKO WASILIANA NASI BOFYA HAPA

Alhamisi, 2 Novemba 2017

 01:14      No comments
Kikosi cha Yanga kitaondoka kesho mapema kwa basi lake kwenda Singida kwa ajili ya mchezo wa Ligi Kuu ya soka Tanzania Bara dhidi ya wenyeji, Singida United Jumamosi Uwanja wa Namfua.

Lakini wachezaji wanne tegemeo hawatakuwepo kwenye msafara huo ambao ni beki Juma Abdul, kiungo Thabani Kamusoko, Donald Ngoma na Mrundi, Amissi Tambwe.

Abdul hatakuwemo kwa sababu anatumikia adhabu ya kadi tatu za njano, wakati Kamusoko, Ngoma na Tambwe wote ni majeruhi wa muda mrefu.

Yanga inaendelea na mazoezi asubuhi ya leo Uwanja wa Uhuru mjini Dar es Salaam kabla ya safari ya kesho kwenda kupambana na timu inayofundishwa na kocha wao wa zamani, Mholanzi, Hans van der Pluijm.

Yanga inakwenda kwenye mchezo huo, ikitoka kutoa sare na wapinzani wa jadi, Simba kwa kufungana 1-1 Jumamosi iliyopita Uwanja wa Uhuru. Sare hiyo imefanya timu hizo ziendelee kufungana kwa pointi 16 kileleni mwa Ligi Kuu.

Ligi Kuu itaendelea Ijumaa, Maji Maji FC wakiikaribisha Stand United Uwanja wa Maji Maji mjini Songea, wakati Jumamosi Singida watakuwa wenyeji wa Yanga Uwanja wa Namfua, Singida na Ndanda FC wataikaribisha Mtibwa Sugar Uwanja wa Nangwanda Sijaona, Mtwara.

Mechi nyingine za Jumamosi, Kagera Sugar wataikaribisha Tanzania Prisons Uwanja wa Kaitaba, Bukoba, Njombe Mji FC wataikaribisha Mbao FC Uwanja wa Saba Saba na Azam FC watakuwa wenyeji wa Ruvu Shooting Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, Dar es Salaam.

Jumapili kutakuwa na mechi mbili ambapo Mbeya City watakipiga na Simba, Lipuli FC nao wataikaribisha Mwadui FC Uwanja wa Samora mjini Iringa.

    0 maoni:

    Chapisha Maoni

    Kurasa

    Translate

    Popular Posts

    Blog Archive

    Tangazo!

    JE UNAHITAJI KUBORESHA BLOG YAKO?

    WEIGHT MANAGEMENT

    WEIGHT MANAGEMENT

    SIKILIZA NYIMBO MPYA

    Watembeleaji

    On Facebook

    Tangazo Victoria!!

    Date & Time

    Weight Management



    CLICK THIS IMAGE

    Sikiliza Clouds Radio



    Sikiliza Kwanza Jamii Radio

    Total Pageviews

    Fomu ya Anwani

    Jina

    Barua pepe *

    Ujumbe *