WELCOME TORINTO HOT MEDIA BLOG | FOR MORE INFORMATION ABOUT OUR NEWS CONTACT US CELL: +255 756 188 180 | Email: josephlieme@gmail.com| KARIBU TORINTO HOT MEDIA BLOG | KWA MAELEZO ZAIDI KUHUSU HABARI ZETU WASILIANA NASI SIMU: +255 756 188 180 | Barua Pepe: josephlieme@gmail.com | DO YOU NEED TO DEVELOP YOUR BLOG CONTACT US CLICK HERE | JE UNAHITAJI KUBORESHA BLOG YAKO WASILIANA NASI BOFYA HAPA

Alhamisi, 2 Novemba 2017

 00:23      No comments
Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam,akifanya uzinduzi katika zoezi la ujenzi WA ofisi za walimu.
RC Makonda akifanya zoezi LA ujenzi baada ya uzinduzi.


Afisa Elimu wilaya ya Ilala akitoa salamu za utambulisho katika eneo LA uzinduzi wa zoezi laA ujenzi WA ofisi za walimu.


Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mheshimiwa PAUL MAKONDA leo amezindua zoezi la ujenzi wa Ofisi za kisasa 402 za Walimu Mkoa wa Dar es Salaam ambapo amesema ujenzi wa Ofisi hizo utaenda kwa kasi ya hali ya juu chini ya Vijana wenye morali ya kazi kutoka JKT, Magereza na Jeshi la Polisi.

Ofisi hizo za kisasa zitakuwa na Ofisi ya Mwalimu Mkuu, Mwalimu Mkuu Msaidizi, Ofisi ya Walimu wa kawaida, Mhasibu, Karani, Chumba cha kuhifadhi Mitihani, Vyoo vya kisasa, Stoo, Jiko, Chumba cha Mikutano na sehemu kuweka Mafaili ambapo ndani ya ofisi zitafungwa AC, Feni, Samani, Taa za kisasa na Umeme.

Akizungumza Katika uzinduzi huo ulioenda sambamba na upandaji wa Miti *RC MAKONDA* amesema kuwa *lengo la ujenzi huo ni kuwezesha Walimu kufanyakazi katika Mazingira mazuri* yatakayowapa morali na hamasa ya kufundisha Wanafunzi.

Aidha MAKONDA amesema kama Walimu wakiboreshewa Mazingira ya kufanya kazi itasaidia kukuza ufaulu.

 MAKONDA amepongeza Walimu kwa kuwezesha Mkoa wa Dar es salaam kushika nafasi ya kwanza kitaifa katika mtihani wa Darasa la saba ikitokea nafasi ya nne mwaka jana na kuwahimiza kukamatia nafasi hiyohiyo.

"Rais MAGUFULI ameshatuonyesha dira kwa kutoa elimu bure na sisi wasaidizi wake ni lazima tuendeleze maono yake, mimi sio kiongozi wa kusubiri kuagizwa ndio nifanye kazi kama ilivyo kwa Remote hadi ibonyezwe ndio ifanye kazi, mimi ni kiongozi wa kujiongeza, sijachaguliwa kuwa mzigo kwa serikali bali kuleta matumaini kwa wananchi"Alisema.

Amewataka Viongozi kuacha Siasa kwenye mambo ya Msingi yanayolenga kuleta maendeleo kwakuwa Maendeleo hayana chama wala ubaguzi wa Dini.

Uzinduzi huo umehudhuriwa na Wakuu wa Wilaya, Kamanda wa Polisi kanda maalumu Dar es Salaam LAZARO MAMBOSASA Kamati ya Ujenzi wa Ofisi za Walimu, Maafisa Elimu, Wakuu wa Shule ambapo Wote kwa pamoja wamepongeza hatua ya MAKONDA kujenga ofisi za Walimu.

0 maoni:

Chapisha Maoni

Kurasa

Translate

Popular Posts

Blog Archive

Tangazo!

JE UNAHITAJI KUBORESHA BLOG YAKO?

WEIGHT MANAGEMENT

WEIGHT MANAGEMENT

SIKILIZA NYIMBO MPYA

Watembeleaji

On Facebook

Tangazo Victoria!!

Date & Time

Weight Management



CLICK THIS IMAGE

Sikiliza Clouds Radio



Sikiliza Kwanza Jamii Radio

Total Pageviews

Fomu ya Anwani

Jina

Barua pepe *

Ujumbe *