WELCOME TORINTO HOT MEDIA BLOG | FOR MORE INFORMATION ABOUT OUR NEWS CONTACT US CELL: +255 756 188 180 | Email: josephlieme@gmail.com| KARIBU TORINTO HOT MEDIA BLOG | KWA MAELEZO ZAIDI KUHUSU HABARI ZETU WASILIANA NASI SIMU: +255 756 188 180 | Barua Pepe: josephlieme@gmail.com | DO YOU NEED TO DEVELOP YOUR BLOG CONTACT US CLICK HERE | JE UNAHITAJI KUBORESHA BLOG YAKO WASILIANA NASI BOFYA HAPA

Jumatatu, 6 Novemba 2017

 23:52      No comments


 
Semina ya utafiti wa kupima matokeo ya elimu
Maofisa Elimu na wakuu wa Shule kutoka Wilaya ya Temeke wakiwa kwenye Semina ya utafiti wa kupima matokeo ya elimu nchini Tanzania iliyoandaliwa na Chuo Kikuu Cha Aga Khan, jijini Dar es Salaam Januari 24, 2017. Picha/ANTHONY SIAME 
Na HADIJA JUMANNE
Imepakiwa - Wednesday, January 25   2017 at  11:02
Kwa Mukhtasari
Chuo Kikuu cha Aga Khan kupitia taasisi ya kuendeleza elimu Afrika Mashariki (IED-EA) wakishirikiana na Chuo Kikuu cha Oxford cha Uingereza wameanza utafiti wa kupima maendeleo ya shule za msingi katika ufundishaji nchini Tanzania.

DAR ES SALAAM, Tanzania
CHUO Kikuu cha Aga Khan kupitia taasisi ya kuendeleza elimu Afrika Mashariki (IED-EA) wakishirikiana na Chuo Kikuu cha Oxford cha Uingereza wameanza utafiti wa kupima maendeleo ya shule za msingi katika ufundishaji nchini.
Utafiti huo pia utafanywa kwa kushirikiana na Chuo Kikuu cha Pretoria cha Afrika Kusini.
Akizindua mradi wa utafiti huo kwa niaba ya Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Mafunzo ya Ufundi Profesa Joyce Ndalichako, Mkurugenzi wa Mafunzo ya Elimu ya Juu kutoka wizara hiyo Profesa Sylivia Temu alisema utafiti huo ni wa miaka mitatu na utatekelezwa katika shule za msingi za Wilaya ya Temeke.
“Kinacholengwa zaidi ni kuwawezesha watoto kuwa na mchango katka mkakati mzima wa kujifunza, waweze kusema ni nini hawakijui na kitu gani wanakijua na wapi wana matatizo ili walimu wajue changamoto kwa ajili ya kufanyia kazi,” alisema Profesa Temu.
Alifafanua kuwa lengo la utafiti huo uliopewa jina la “Kupima kwa ajili ya kujifunza Afrika” (Afla) ni kusaidia wanafunzi kuelewa masomo yao.
“Utafiti huo ambao umelenga somo la Hisabati umeanza kutekelezwa katika shule zote za msingi zilizopo wilayani Temeke wakishirikiana na Chuo cha Ualimu Vikindu,” alisema Profesa Temu.

0 maoni:

Chapisha Maoni

Kurasa

Translate

Popular Posts

Blog Archive

Tangazo!

JE UNAHITAJI KUBORESHA BLOG YAKO?

WEIGHT MANAGEMENT

WEIGHT MANAGEMENT

SIKILIZA NYIMBO MPYA

Watembeleaji

On Facebook

Tangazo Victoria!!

Date & Time

Weight Management



CLICK THIS IMAGE

Sikiliza Clouds Radio



Sikiliza Kwanza Jamii Radio

Total Pageviews

Fomu ya Anwani

Jina

Barua pepe *

Ujumbe *