WELCOME TORINTO HOT MEDIA BLOG | FOR MORE INFORMATION ABOUT OUR NEWS CONTACT US CELL: +255 756 188 180 | Email: josephlieme@gmail.com| KARIBU TORINTO HOT MEDIA BLOG | KWA MAELEZO ZAIDI KUHUSU HABARI ZETU WASILIANA NASI SIMU: +255 756 188 180 | Barua Pepe: josephlieme@gmail.com | DO YOU NEED TO DEVELOP YOUR BLOG CONTACT US CLICK HERE | JE UNAHITAJI KUBORESHA BLOG YAKO WASILIANA NASI BOFYA HAPA

Jumatano, 4 Oktoba 2017

 03:18      No comments

TAARIFA KUHUSIANA NA SEMINA ENDELEVU YA YA 28, ITAKAYOFANYIKA TAREHE 12-13 OCTOBER,2017 KATIKA UKUMBI WA MLIMANI CITY– DAR ES SALAAM.


  Na Torinto Hot Blog.
Albert Munuo

KAIMU MSAJILI BODI YA USAJILI WA WABUNIFU MAJENGONA WAKADIRIAJI MAJENZI

















1.0    UTANGULIZI:

Bodi ya Usajili wa Wabunifu Majengo na Wakadiriaji Majenzi ni taasisi ya Serikali chini ya Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano inayosimamia utekelezaji wa sheria namba 4 ya mwaka 2010.

Jukumu kuu la Bodi ni kusajili na kuratibu mienendo ya kitaalam ya Wabunifu Majengo, Wakadiriaji Majenzi, Wataalam wanaohusiana nao pamoja na kampuni zao.

Pamoja na majukumu mengine yaliyoainishwa katika kifungu cha 5 cha sheria hiyo, Bodi ina wajibu wa kuratibu na kutoa nafasi za mafunzo endelevu kwa wadau wa sekta ya ujenzi kupitia semina na warsha mbalimbali.

Semina hizi zilianzishwa mwaka 2003 na hufanyika mara mbili kwa mwaka. Jumla ya wadau 5,789 wa sekta ya ujenzi wamenufaika na semina hizi.



Albert Munuo

KAIMU MSAJILI BODI YA USAJILI WA WABUNIFU MAJENGONA WAKADIRIAJI MAJENZI










Semina ya 28 itakuwa ni ya siku mbili, tarehe 12 na 13 October,2017, kuanzia saa 1.30 asubuhi,na Mgeni Rasmi atakuwa Mheshimiwa Professa Makame Mbarawa(MB), Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano;

2.0    MALENGO MAKUBWA YA SEMINA HII:

·        Kuwanoa Wabunifu Majengo(Architects), Wasanifu wa Ndani ya Majengo( Interior Designers), Wabunifu wa Mandhari ya Nje(Landscape Architects), Wakadiriaji Majenzi(Quantity Surveyors), Wasimamizi Ujenzi( Construction Managers), Watathmini Majengo(Building Surveyors) na wadau wengine katika sekta ya ujenzi kukabiliana na mabadiliko ya sayansi na teknolojia katika sekta ya ujenzi.
·        Kubadilishana uzoefu wa kazi za kitaalam kwa lengo la kuziboresha.
·        Kuwapa fursa wataalam katika sekta ya ujenzi kupata nasaha kutoka kwa viongozi wa serikali.

3.0     Mada Kuu ni Mbinu za Kupunguza Madhara ya Matetemeko ya Ardhi, Ukaguzi wa Miradi ya Ujenzi na Matengenezo ya Majengo na Miundombinu Katika Sekta ya Ujenzi (Mitigation of Earthquakes, Technical Audits and Maintenance in The Construction Industry)

Mada zifuatazo zitatolewa:
1.   Consideration of Earthquakes Forces in Structure Design in Tanzania
2.   Technical Audits in the Construction Industry.
3.   Maintenance of Construction Projects.
4.   Project Cost Accounting in Professional Practice in the Construction Industry.

Mada hizi zimechaguliwa kuwapa fursa wadau katika sekta ya ujenzi, kukumbushana umuhimu wa mambo yafuatayo:
(i)         Kukuza uelewa wa kitaalam kuhusu namna ya kuzingatia tatizo la matetemeko ya ardhi katika Ubunifu, Ukadiriaji na Ujenzi wa majengo na miundo mbinu, ili kupunguza athari zinazoweza kuletwa na matetemeko kwenye miradi ya ujenzi, wakati wa ujenzi na wakati wa matumizi ya jengo. Mada hii imebuniwa kufuatia matetemeko yaliyotokea sehemu mbali mbali duniani, ikiwepo Kagera na kusababisha maafa makubwa kwa jamii.
(ii)        Kukuza uelewa wa namna ya kufanya ukaguzi wa miradi ya ujenzi katika hatua mbali mbali.
(iii)      Umuhimu wa kuzingatia ukarabati katika miradi ya ujenzi, ili kuongeza thamani ya miradi na kupunguza gharama za matengenezo, pale inapoachwa kwa muda mrefu bila matengenezo. Tukumbuke kauli ya wahenga isemayo ‘usipoziba ufa utajenga ukuta’; na hili limetokea kwa mradi mingi ya ujenzi.
(iv)      Kuelimisha wadau kuelewa namna ya kupanga gharama za uendeshaji wa miradi, ili kuepusha gharama na hasara zisizo za lazima wakati wa ujenzi wa miradi.

4.0    HITIMISHO:
Bodi inachukua fursa hii kuwasihi Wabunifu Majengo, ‘Interior Designers’ ‘Landsacpe Architects’ , Wakadiriaji Majenzi, ‘Building Surveyors’ ‘Construction Managers’ ‘Project Managers’ Wahandisi, Wakandarasi na wadau wengine katika sekta ya ujenzi kushiriki kwa wingi katika semina hii muhimu, ili kuwaongezea ujuzi na maarifa ya kuboresha utendaji wao wa kazi.

Bodi inapenda kuwaomba waajiri wote nchini kufadhili kwa kuwalipia wataalam wao ada ya shs 300,000, ili waweze kuhudhuria semina hii, ambayo itawawezesha wataalam wao kuongeza tija katika utendaji wao wa kazi.

Aidha napenda kuwakaribisha wanahabari katika semina; ili kuwezesha wananchi kupata habari zaidi juu ya semina hii.




0 maoni:

Chapisha Maoni

Kurasa

Translate

Popular Posts

Blog Archive

Tangazo!

JE UNAHITAJI KUBORESHA BLOG YAKO?

WEIGHT MANAGEMENT

WEIGHT MANAGEMENT

SIKILIZA NYIMBO MPYA

Watembeleaji

On Facebook

Tangazo Victoria!!

Date & Time

Weight Management



CLICK THIS IMAGE

Sikiliza Clouds Radio



Sikiliza Kwanza Jamii Radio

Total Pageviews

Fomu ya Anwani

Jina

Barua pepe *

Ujumbe *