WELCOME TORINTO HOT MEDIA BLOG | FOR MORE INFORMATION ABOUT OUR NEWS CONTACT US CELL: +255 756 188 180 | Email: josephlieme@gmail.com| KARIBU TORINTO HOT MEDIA BLOG | KWA MAELEZO ZAIDI KUHUSU HABARI ZETU WASILIANA NASI SIMU: +255 756 188 180 | Barua Pepe: josephlieme@gmail.com | DO YOU NEED TO DEVELOP YOUR BLOG CONTACT US CLICK HERE | JE UNAHITAJI KUBORESHA BLOG YAKO WASILIANA NASI BOFYA HAPA

Jumatano, 30 Mei 2018

 04:21      No comments




NA Joseph Maiko
Vipodozi vilivyopigwa mrufuku vyenye thamani ya milioni 72,406,500 pamoja na Pombe kali zilizopigwa marufuku zenye thamani ya Milioni 11,356,000 vimekamatwa vikiwa kwenye maduka mbali mbali kwa ajili ya kuuziwa wananchi.


Hayo yamebainishwa leo Jijni Dar es Salaam na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA) ,Bi Agnes Kijo ,wakati wa alipokuwa anatoa taarifa kwa waandishi wa Habari kuhusu  ukaguzi maalum wa kukagua na kuondoa katika soko  vipodozi visivyosajiliwa,pombe kali zisizosajiliwa pamoja na kufuatilia uhalali wa biashara ya vipodozi kwenye mitandao ya kijamii.


Ambapo, Bi Kijo amesema katika Ukaguzi huo ambao ulishirikisha Jeshi la Polisi,TFDA,Shirika la Viwango nchini (TBS),Wakala  wa Mkemia Mkuu wa Serikali (GCLA) na Ofisi ya Rais,


Amesema katika ukaguzi huo ulifanyika katika mikoa ya Dar es Salaam,Pwani,Mwanza,Shinyanga,Geita,Mara na Arusha ambapo ukaguzi huo ulichukua mda wa siku mbili.


Bi Kijo amevitaja vipodozi vilivyokamatwa ni Carolight cream,Citrolight Crem,Sivoclaire Cream,Max light cream,dawa zinazodaiwa kuongeza maumbile kwa wanaume(Maxman capsules) sabani za kurudisha usichana ( Virginity soap).


 Vipodozi vengine ni Dawa za kuongeza ukubwa wa maziwa kwa wanawake (Papaya breast enlarging crem) pamoja na dawa za kutibu magonjwa ambazo zimekuwa zikitumika kimakosa.


Sanjari na Vipodozi hivyo vilivyopigwa marufuku pia katika ukaguzi huo wamekatamata  pombe kali zenye ujazo milimita 200  ambazo  zinazofungashwa kwenye viroba.


"Tumekamata pombe hizi ni imperial blue whsky,White mischief vodka,contessa preimium dry gin vodka,Konyagi (Ladha ya pesheni)magic movement vodka,officers choice ,Dewer's white label,Officers can spirit,sinature vodk "amesema Bi Kijo.




Hata hivyo Bi Kijo amesema baada ya ukaguzi huo  wamechukua hatua mbali mbali ikiwemo kufunga majadala 24 ya kesi katika vituo mbali mbali vya  Polisi dhidi ya watuhumiwa  na majengo ya biashara 29 yamefungwa.
"Baada ya uchunguzi wa makosa kukamilika hatua  mbali mbali zinatachukuliwa ikiwa ni pamoja kukamilika kwa hatua mbali zitachukuliwa ikiwa ni  pamoja na kuwapeleka mhakamani watuhumiwa na kutoa dhabu kulingana na sheria ya Chakula,Dawa na Vipodozi ,Sura  219"


"Adhabu hizo zinajumuisha kufutwa leseni ya biashara na kuharibu bidhaa zilizokamatwa kwa gharama ya mtuhimiwa"amesema


Bi Kijo amewataka wananchi kuendendelea kutoa taarifa za wale wote wanaojihusisha na biashara ya vipodozi vilivyopigwa marufuku ,Biashara harany ya vipodozi na dawa katika mitandao ya kijamii ili hatua zichukuliwe na Mamlaka husika.




0 maoni:

Chapisha Maoni

Kurasa

Translate

Popular Posts

Blog Archive

Tangazo!

JE UNAHITAJI KUBORESHA BLOG YAKO?

WEIGHT MANAGEMENT

WEIGHT MANAGEMENT

SIKILIZA NYIMBO MPYA

Watembeleaji

On Facebook

Tangazo Victoria!!

Date & Time

Weight Management



CLICK THIS IMAGE

Sikiliza Clouds Radio



Sikiliza Kwanza Jamii Radio

Total Pageviews

Fomu ya Anwani

Jina

Barua pepe *

Ujumbe *