WELCOME TORINTO HOT MEDIA BLOG | FOR MORE INFORMATION ABOUT OUR NEWS CONTACT US CELL: +255 756 188 180 | Email: josephlieme@gmail.com| KARIBU TORINTO HOT MEDIA BLOG | KWA MAELEZO ZAIDI KUHUSU HABARI ZETU WASILIANA NASI SIMU: +255 756 188 180 | Barua Pepe: josephlieme@gmail.com | DO YOU NEED TO DEVELOP YOUR BLOG CONTACT US CLICK HERE | JE UNAHITAJI KUBORESHA BLOG YAKO WASILIANA NASI BOFYA HAPA

Jumanne, 21 Machi 2017

 02:14      No comments


 TAGS
“Sisi kama Serikali tunalaani kilichotokea. Kwenye nchi ambayo imesaini mikataba ya kimataifa ya uhuru wa habari, na nchi yenye Katiba inayolinda vyombo vya habari; hiki kilichotokea ni kunajisi Uhuru wa habari.
Kabla ya kuchukua hatua zozote, sisi kama Serikali tunataka kusikia kutoka kwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda. Tumeunda timu ya watu 5 kufanya kazi kwa saa 24 ili wapate maelezo ya Mkuu wa Mkoa. Baada ya hapo tutasema hatua tutakazochukua (kama Serikali) “
” I am very proud of you ( #CloudsMediaGroup ), jambo hili mmelipeleka in a very professional way.
Jambo lilitokea lilikuwa kubwa na la kutisha lakini mpaka J1 mlitulia kama hakuna kilichotokea. Hali ilikuwa mbaya nilishapata taarifa kutoka kwa Waandishi wa mikoani wakitaka kuandamana. Lakini ninyi mmelinda amani ya nchi yetu na mkalipeleka jambo kwa utaratibu mzuri “
Kwa upande wake Mkurugenzi wa Makampuni ya IPP Regnald Mengi ambaye pia ni Mwenyekiti wa wamiliki wa vyombo vya habari (MOAT) ameeleza yafuatayo.
“Jambo lililofanyika ni la hatari sana. Na lazima tujiulize mtu huyu ( Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam ) anapata wapi ujasiri huu?. Kama alikuja na bunduki hapa anaweza kwenda nazo popote na pengine kuna siku atazitumia.
Mimi nina imani kwamba tuna Rais anayetupenda sana, na tuna Waziri anayetupenda sana. Lakini mapenzi hayo lazima yaonyeshwe kwa vitendo.
” Sura moja ya muandishi wa habari ni kutokuwa muoga. Jambo hili lililotokea lisifanye tukawa waoga. Wanahabari sio waoga.”
“Jambo lililofanyika ni la hatari sana. Na lazima tujiulize mtu huyu ( Mkuu wa Mkoa wa DSM ) anapata wapi ujasiri huu?
Kama alikuja na bunduki hapa anaweza kwenda nazo popote na pengine kuna siku atazitumia.”
@josephkusaga ni Mtoto wangu ninayempenda sana. Kuna wakati nilitaka ‘kumuadopt’ lakini akasema sasa jina langu itakuwaje? . Hilo lilishindikana lakini ni mwanangu, ninampenda sana “

0 maoni:

Chapisha Maoni

Kurasa

Translate

Popular Posts

Blog Archive

Tangazo!

JE UNAHITAJI KUBORESHA BLOG YAKO?

WEIGHT MANAGEMENT

WEIGHT MANAGEMENT

SIKILIZA NYIMBO MPYA

Watembeleaji

On Facebook

Tangazo Victoria!!

Date & Time

Weight Management



CLICK THIS IMAGE

Sikiliza Clouds Radio



Sikiliza Kwanza Jamii Radio

Total Pageviews

Fomu ya Anwani

Jina

Barua pepe *

Ujumbe *