WELCOME TORINTO HOT MEDIA BLOG | FOR MORE INFORMATION ABOUT OUR NEWS CONTACT US CELL: +255 756 188 180 | Email: josephlieme@gmail.com| KARIBU TORINTO HOT MEDIA BLOG | KWA MAELEZO ZAIDI KUHUSU HABARI ZETU WASILIANA NASI SIMU: +255 756 188 180 | Barua Pepe: josephlieme@gmail.com | DO YOU NEED TO DEVELOP YOUR BLOG CONTACT US CLICK HERE | JE UNAHITAJI KUBORESHA BLOG YAKO WASILIANA NASI BOFYA HAPA

Jumanne, 7 Novemba 2023

 06:44      No comments

 Torintohot media Blog

Jerome Mlaki wa Dar 



Na Mwandishi wetu 

UJENZI WA MRADI WA BOMBA LA MAFUTA LA HOIMA UNASHIRIKISHA WAZAWA MKOANI KAGERA #Wakandarasi na wa watoa huduma 42 wapatiwa kazi Dodoma 

Imeelezwa kuwa ujenzi wa Mradi wa bomba la mafuta kutoka Hoima nchini Uganda hadi Chongoleani mkoani Tanga unashirikisha wakandarasi wazawa kutoka mkoani Kagera. 

Hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa Nishati Mhe. Judith Kapinga, kwa niaba ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Mhe. Dkt. Doto Biteko wakati alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa viti maalumu kutoka mkoani Kagera Mhe. Neema Kichiki Lugangira aliyetaka kujua je ni wakandarasi wangapi kutoka mkoani Kagera wamepata kazi katika mnyororo wa ujenzi wa bomba la mafuta la Hoima mkoani Tanga. 

Mhe. Kapinga amesema kuwa wakandarasi wakuu wa Mradi wa ujenzi wa bomba la mafuta kutoka Hoima nchini Uganda hadi Chongoleani mkoani Tanga wanaendelea kushirikiana na wakandarasi wadogo, wajenzi na na wanna huduma mbalimbali katika mikoa yote inayopitiwa na Mradi. 

Mhe. kapinga aliongeza kuwa jumla ya wakandarasi na watoa huduma 42 wamepata kazi mbalimbali katika mnyororo wa thamani wa ujenzi wa Mradi huu ikiwemo uuzaji wa vifaa vya ujenzi, huduma za usambazaji wa mafuta, huduma za umeme na hoteli.


0 maoni:

Chapisha Maoni

Kurasa

Translate

Popular Posts

Blog Archive

Tangazo!

JE UNAHITAJI KUBORESHA BLOG YAKO?

WEIGHT MANAGEMENT

WEIGHT MANAGEMENT

SIKILIZA NYIMBO MPYA

Watembeleaji

On Facebook

Tangazo Victoria!!

Date & Time

Weight Management



CLICK THIS IMAGE

Sikiliza Clouds Radio



Sikiliza Kwanza Jamii Radio

Total Pageviews

Fomu ya Anwani

Jina

Barua pepe *

Ujumbe *