WELCOME TORINTO HOT MEDIA BLOG | FOR MORE INFORMATION ABOUT OUR NEWS CONTACT US CELL: +255 756 188 180 | Email: josephlieme@gmail.com| KARIBU TORINTO HOT MEDIA BLOG | KWA MAELEZO ZAIDI KUHUSU HABARI ZETU WASILIANA NASI SIMU: +255 756 188 180 | Barua Pepe: josephlieme@gmail.com | DO YOU NEED TO DEVELOP YOUR BLOG CONTACT US CLICK HERE | JE UNAHITAJI KUBORESHA BLOG YAKO WASILIANA NASI BOFYA HAPA

Alhamisi, 3 Agosti 2017

 03:15      No comments


jag1
Waziri wa Biashara na Viwanda wa Vietnam Mhe. Tran Tuan akisalimiana na Waziri wa Kilimo na Chakula  Mh. Charles Tizeba Katikati ni Waziri wa Viwanda na Biashara Mh. Charles Mwijage.
jag4
Wakiwa katika mkutano
jag5
Wakiwa katika picha ya pamoja.
…………………………………………………………………………….
Tarehe 2 Agosti, 2017, ikiwa ni siku ya tatu ya ziara yao nchini Vietnam, Mhe. Charles Mwijage, (Mb.) Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji na Mhe. Dkt. Charles Tizeba, Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi wamekutana kwa mazungumzo na Mhe. NGUYEN XUAN PHUC, Waziri Mkuu wa Vietnam ambapo walijadili namna ya kuimarisha mahusiano na ushirikiano wa kiuchumi na biashara baina ya nchi hizo mbili. Mazungumzo hayo yalifanyika mara baada ya kukamilisha kongamano la tatu la biashara na uwekezaji kati ya Tanzania na Vietnam lililofanyika siku hiyo hiyo ya tatu ya ziara yao.
Katika mazungumzo yao, Mheshimiwa Waziri Mkuu wa Vietnam aliipongeza Serikali ya Tanzania kwa hatua nzuri za kiuchumi inazoendelea kupiga kwa kuzingatia kwamba Tanzania ni kati ya nchi kumi duniani ambazo uchumi wake unakua kwa kasi na ni ya kwanza kwa Afrika Mashariki. Aliishukuru pia serikali ya Tanzania kwa kuendelea kuisaidia kampuni ya Halotel katika utoaji wa huduma zake za mawasiliano na hasa vijijini. Aliwakikishia Washemiwa Mawaziri hao kuwa Vietnam itaendelea kushirikiana na Tanzania ili kuhakikisha kuwa nchi hizo zinafikia malengo ya biashara yaliyowekwa na Waheshimiwa Marais wa nchi hizi hapo mwaka 2016 nchini Tanzania.
Kwa upande wake Mhe. Mwijage alieleza kuwa Serikali ya Tanzania inatambua na kuenzi urafiki na ushirikiano wa muda mrefu kati ya nchi hizi mbili. Alieleza kuwa lengo la ziara hiyo ni kuendeleza mikakati ya kutekeleza maelekezo ya viongozi wa nchi hizo mbili kwamba ifikapo mwaka 2020 biashara kati ya nchi hizi ifikie dola za marekanii bilioni 1. Hivyo, kongamano la uwekezaji lililofanyika hapo mjini Hanoi, limeweza kuwakutanisha wafanyabiashara wa Tanzania wapatao 30 na wafanyabiashara wa Vietnam zaidi ya 200. Aidha, kutokana na kongamano hilo, changamoto mbalimbali zilielezwa ambazo zinarudisha nyuma jitihada za wafanyabiasha. Alieleza kuwa tayari amekutana na Waziri wa Biashara na Biwanda wa Vietnam na wamekubaliana timu ya wataalmu ikutane Dar es Salaam mwezi Septemba kuanza kufanyia kazi mapungufu hayo kwa pande za nchi zote.
Nae Mhe. Tizeba alimshukuru Mheshimiwa Waziri Mkuu kwa nafasi aliyowapa ya kukutana pamoja na kuwa ana majukumu mengi. Alieleza kuwa changaoto nyingi zilizoelezwa na wafanyabiashara katika kongamano la biashara zingeweza kutatuliwa iwapo hati za makubaliano zilizopendekezwa na nchi hizo zingekuwa zimekamilishwa na kuwekwa saini. Hivyo, alimuomba Mheshimiwa Waziri Mkuu asaidie kwa upande wa Serikali ya Vietnam ili hati za makubaliano ya ushirikiano kati ya taasisi mbali mbali za Tanzania na Vietnam zikamilishe na kurahisisha biashara.

0 maoni:

Chapisha Maoni

Kurasa

Translate

Popular Posts

Blog Archive

Tangazo!

JE UNAHITAJI KUBORESHA BLOG YAKO?

WEIGHT MANAGEMENT

WEIGHT MANAGEMENT

SIKILIZA NYIMBO MPYA

Watembeleaji

On Facebook

Tangazo Victoria!!

Date & Time

Weight Management



CLICK THIS IMAGE

Sikiliza Clouds Radio



Sikiliza Kwanza Jamii Radio

Total Pageviews

Fomu ya Anwani

Jina

Barua pepe *

Ujumbe *