WELCOME TORINTO HOT MEDIA BLOG | FOR MORE INFORMATION ABOUT OUR NEWS CONTACT US CELL: +255 756 188 180 | Email: josephlieme@gmail.com| KARIBU TORINTO HOT MEDIA BLOG | KWA MAELEZO ZAIDI KUHUSU HABARI ZETU WASILIANA NASI SIMU: +255 756 188 180 | Barua Pepe: josephlieme@gmail.com | DO YOU NEED TO DEVELOP YOUR BLOG CONTACT US CLICK HERE | JE UNAHITAJI KUBORESHA BLOG YAKO WASILIANA NASI BOFYA HAPA

Alhamisi, 3 Agosti 2017

 02:55      No comments


 TAGS
Msajili wa Vyama vya Siasa nchini, Jaji Francis Mutungi amepinga maamuzi ya Chama Cha Wananchi (CUF) kuwafukuza Uanachama Wabunge wawili wa chama  hicho Magdalena Sakaya na Maftaha Nachuma na kusema Maalim Seif hatambuliki kama Katibu Mkuu wa CUF.

Msajili wa Vyama vya Siasa amesema hayo leo wakati akijibu barua iliyowasilishwa ofisini kwake na Katibu Mkuu wa (CUF) Maalim Seif Sharif Hamad akimtaka msajili wa vyama kuwavua nafasi ya Ubunge viongozi hao.

Kufuatia barau hiyo Msajili wa Vyama Vya Siasa amesema kuwa hamtambui Maalim Seif Sharif Hamad kama Katibu Mkuu wa CUF na kusema yeye anawatambua Mwenyekiti wa CUF, Professa Ibrahim Lipumba pamoja na Magdalena Sakaya kama mtu mwenye dhamana ya Katibu Mkuu wa CUF

Chama Cha Wananchi (CUF) kipo katika mgogoro wa pande mbili upande wa Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif pamoja na upande wa Mwenyekiti wa CUF anayetambuliwa na Msajili wa Vyama Vya Siasa nchini Profesa Ibrahim Lipumba, kufuatia mgogoro huo mpaka sasa kuna kesi mbalimbali ambazo zimefunguliwa mahakamani kutokana na mvutano wa pande hizo zote mbili. 
 ==>Hapo chini ni barua ya msaili wa vyama akijibu bara ya Maalim Seif

0 maoni:

Chapisha Maoni

Kurasa

Translate

Popular Posts

Blog Archive

Tangazo!

JE UNAHITAJI KUBORESHA BLOG YAKO?

WEIGHT MANAGEMENT

WEIGHT MANAGEMENT

SIKILIZA NYIMBO MPYA

Watembeleaji

On Facebook

Tangazo Victoria!!

Date & Time

Weight Management



CLICK THIS IMAGE

Sikiliza Clouds Radio



Sikiliza Kwanza Jamii Radio

Total Pageviews

Fomu ya Anwani

Jina

Barua pepe *

Ujumbe *