WELCOME TORINTO HOT MEDIA BLOG | FOR MORE INFORMATION ABOUT OUR NEWS CONTACT US CELL: +255 756 188 180 | Email: josephlieme@gmail.com| KARIBU TORINTO HOT MEDIA BLOG | KWA MAELEZO ZAIDI KUHUSU HABARI ZETU WASILIANA NASI SIMU: +255 756 188 180 | Barua Pepe: josephlieme@gmail.com | DO YOU NEED TO DEVELOP YOUR BLOG CONTACT US CLICK HERE | JE UNAHITAJI KUBORESHA BLOG YAKO WASILIANA NASI BOFYA HAPA

Jumatano, 29 Machi 2017

 05:04      No comments


WA
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo Ndg John Lipesi Kayombo ambaye kachaguliwa kuwa MUWEKA HAZINA wa Wakurugenzi nchini
Mkurugenzi wa Jiji la Mwanza Ndg Kiomoni Kibamba, ambaye kachaguliwa kuwa Mwenyekiti wa Wakurugenzi nchini
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Same Ndg Anne Claire Shija (Kushoto) ambaye kachaguliwa kuwa katibu wa Wakurugenzi nchini
Na Mathias Canal, Dodoma
Wakurugenzi wa Halmashauri za Wilaya na Manispaa kote nchini kwa kauli moja wameridhia na kuwachagua viongozi watakaowawakilisha katika kufikisha changamoto zao mbalimbali katika ngazi za juu ili kupungunza uwasilishaji wa kila Mkurugenzi kufikisha changamoto zake ngazi za juu.
Uchaguzi huo umefanyika hii Leo katika ukumbi wa Hazina Mjini Dodoma kwa maridhiano ya Wakurugenzi wote kwa asilimia 100% ya kura zote.
Uchaguzi huo umejili Mara baada ya kumalizika kikao cha kazi kilichoongozwa na Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na serikali za mitaa (TAMISEMI) Eng Musa Iyombe kilichohudhuriwa na Wakurugenzi wote 185.
Wakurugenzi hao wamefanya uchaguzi kwa nafasi nne ambazo ni Mwenyekiti na Makamu Mwenyekiti sambamba na Katibu pamoja na Muweka Hazina.
Wakurugenzi waliochaguliwa katika nafasi hizo ni
1. Mkurugenzi wa Jiji la Mwanza Ndg Kiomoni Kibamba, ambaye kachaguliwa kuwa Mwenyekiti
2. Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Bahi Ndg Rachel Chuwa ambaye kachaguliwa kuwa Makamu Mwenyekiti.
3. Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Same Ndg Anne Claire Shija, ambaye kachaguliwa kuwa katibu. Na
4. Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo
Ndg John Lipesi Kayombo ambaye kachaguliwa kuwa MUWEKA HAZINA
Wakizungumza kwa nyakati tofauti Mara baada ya uchaguzi huo kumalizika Viongozi hao waliochaguliwa wameeleza namna bora ya kuhumiza uwajibikaji kwa Wakurugenzi wote sambamba na kuwawakilisha vyema kufikisha changamoto zao kwa ngazi za juu.
Wameueleza mtandao wa www.wazo-huru.blogspotm.com kuwa imani kubwa waliyopatiwa na Wakurugenzi wote nchini ya kuwachagua kuwa wawakilishi wao ni kubwa hivyo wana kila sababu ya kuitumikia kwa weledi na usawa.
“Kupitia Wawakilishi hao waliochaguliwa Wakurugenzi nchini wataraji utendaji uliotukuka na uwakilishi unaostahili kulingana na changamoto zinazowakabili katika maeneo yao” Alisema MD Kayombo John L.

0 maoni:

Chapisha Maoni

Kurasa

Translate

Popular Posts

Blog Archive

Tangazo!

JE UNAHITAJI KUBORESHA BLOG YAKO?

WEIGHT MANAGEMENT

WEIGHT MANAGEMENT

SIKILIZA NYIMBO MPYA

Watembeleaji

On Facebook

Tangazo Victoria!!

Date & Time

Weight Management



CLICK THIS IMAGE

Sikiliza Clouds Radio



Sikiliza Kwanza Jamii Radio

Total Pageviews

Fomu ya Anwani

Jina

Barua pepe *

Ujumbe *