WELCOME TORINTO HOT MEDIA BLOG | FOR MORE INFORMATION ABOUT OUR NEWS CONTACT US CELL: +255 756 188 180 | Email: josephlieme@gmail.com| KARIBU TORINTO HOT MEDIA BLOG | KWA MAELEZO ZAIDI KUHUSU HABARI ZETU WASILIANA NASI SIMU: +255 756 188 180 | Barua Pepe: josephlieme@gmail.com | DO YOU NEED TO DEVELOP YOUR BLOG CONTACT US CLICK HERE | JE UNAHITAJI KUBORESHA BLOG YAKO WASILIANA NASI BOFYA HAPA

Ijumaa, 28 Oktoba 2016

 06:45      No comments


Tarehe 26/10/2016 nyenzo ya mawasiliano inayotumiwa na Mradi wa Lishe wa Mwanzao Bora ili

kuboresha lishe ya akina mama na watoto itaasiliwa na Serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania

ili kuwa kama nyenzo ya kitaifa. Nyenzo hii inayoitwa "Mkoba wa siku 1000" itazinduliwa katika

ukumbi wa kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere kama sehemu ya mkutano shirikishi wa tathmini ya

lishe wa mwaka 2016. Mwanzo Bora ni mradi wa lishe wa miaka saba unaofadhiliwa na Watu wa

Marekani kupitia Shirika la Maendeleo la Marekani (USAID). Mradi wa lishe wa Mwanzo Bora una

lengo la kupunguza kwa asilimia 20 udumavu kwa watoto wenye umri chini ya miaka miwili na pia

upungufu wa damu kwa akinamama wajawazito na wanaonyonyesha katika mikoa sita ya Tanzania Bara

na katika wilaya tatu ya Zanzibar.

Inakadiriwa kuwa watoto milioni 2.7 hapa nchini Tanzania walio chini ya umri wa miaka mitano

wamedumaa. Juhudi zinazofanywa na serikali pamoja na wadau mbalimbali wa masuala ya lishe

zinasaidia sana katika kupunguza tatizo la udumavu; kwani tatizo hili limepungua kwa kiasi kikubwa

kutoka asilimia 42 (mwaka 2010) mpaka kufikia asilimia 35 (mwaka 2015).

Kupungua kwa tatizo la udumavu hapa nchini kumechangiwa pia na matumizi ya Mkoba wa Siku 1000

uliotengenezwa na mradi wa lishe wa Mwanzo Bora kwa kushirikiana na Taasisi ya Chakula na Lishe

Tanzania. Mradi wa lishe wa Mwanzo Bora umechangia pia kwa kiasi kikubwa kupunguza tatizo la

udumavu katika mikoa ya Dodoma (kutoka asilimia 56 mpaka asilimia 36.5), Morogoro (kutoka asilimia

44 mpaka asilimia 33.4) na Manyara (kutoka asilimia 56 mpaka asilimia 36.5).Mafanikio haya

yametokana na matumizi ya Mkoba wa Siku 1000 ambao unahamasisha mabadiliko ya tabia za lishe.

Mkoba wa Siku 1000 utaasiliwa na Serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania kama mkoba

maalumu wa kitaifa utakaotumika kutekeleza afua mbalimbali za lishe hapa nchini. Mradi wa lishe wa

Mwanzo Bora utakabidhi mikoba 200 kwa Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania.ambapo mwakilishi

kutoka Taasisi ya Chakula na Lishe atakabidhi mikoba hiyo kwa Kaimu Katibu Mkuu Ofisi ya Raisi

kama mwakilishi wa serikali. Tendo hili litamaanisha kwamba Mkoba wa Siku 1000 umezinduliwa rasmi

kuwa mkoba wa Kitaifa.

Baada ya uzinduzi huu, Mkoba wa Siku 1000 na wadau mbalimbali wa lishe hapa nchini kama vile

maafisa lishe wa mikoa na wilaya pamoja na taasisi na mashirika mbalimbali ili kuhamasisha tabia

chanya za lishe na hivyo kupunguza tatizo la udumavu kwa watoto na upungufu wa damu kwa

akinamama wajawazito na wanaonyonyesha katika jamii zetu.Mkazo unawekwa katika kuhamasisha tabia

na mitazamo ya kijinsia itakayosaidia kuboresha hali za lishe na afya za akinamama na watoto.

Uzinduzi wa Mkoba wa Siku 1000 umeandaliwa na Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania.Washiriki

katika uzinduzi huu wanajumuisha wadau kutoka katika mashirika yasiyo ya kiserikali pamoja na wadau

wengine wa masuala ya lishe

0 maoni:

Chapisha Maoni

Kurasa

Translate

Popular Posts

Blog Archive

Tangazo!

JE UNAHITAJI KUBORESHA BLOG YAKO?

WEIGHT MANAGEMENT

WEIGHT MANAGEMENT

SIKILIZA NYIMBO MPYA

Watembeleaji

On Facebook

Tangazo Victoria!!

Date & Time

Weight Management



CLICK THIS IMAGE

Sikiliza Clouds Radio



Sikiliza Kwanza Jamii Radio

Total Pageviews

Fomu ya Anwani

Jina

Barua pepe *

Ujumbe *