WELCOME TORINTO HOT MEDIA BLOG | FOR MORE INFORMATION ABOUT OUR NEWS CONTACT US CELL: +255 756 188 180 | Email: josephlieme@gmail.com| KARIBU TORINTO HOT MEDIA BLOG | KWA MAELEZO ZAIDI KUHUSU HABARI ZETU WASILIANA NASI SIMU: +255 756 188 180 | Barua Pepe: josephlieme@gmail.com | DO YOU NEED TO DEVELOP YOUR BLOG CONTACT US CLICK HERE | JE UNAHITAJI KUBORESHA BLOG YAKO WASILIANA NASI BOFYA HAPA

Jumatatu, 6 Novemba 2017

 04:06      No comments

Afisa mwandamizi wa soko la Hisa Dar es salaam Bi Mary Kinabo akizungumza na vyombo vya habari leo hii.

             Na Joseph Lieme-Dar 

SOKO la Hisa  Dar es Salaam(DSE) limesema thamani ya mauzo ya hisa imepungua kutoka Sh bilioni 20  kwa wiki iliyoishia Oktoba 27 hadi Sh bilioni 3 ya wiki iliyoishia Novemba 3 mwaka huu.

Hayo yamesemwa leo jijini humo na Afisa Mwandamizi Masoko wa Dar es Salaam wa DSE, Mary Kinabo wakati anawasilisha yaliyojiri kwenye soko hilo kwa wiki iliyoishia Novemba 3 mwaka huu.

Amesema idadi ya hisa zilizouzwa na kununuliwa imepanda kutoka hisa milioni 1.6 ya wiki iliyoishia Oktoba 27 hadi hisa milioni 3.5 ya wiki iliyoishia tarehe 3 mwezi Novemba, 2017.

" Kampuni zilizoongoza katika mauzo ya soko la hisa ni TCC (41%), Tanzania Breweweries  Ltd (27%), Benki ya CRDB (16%) na VODA (11%), amesema.

Amebainisha kuwa ukubwa wa mtaji wa kampuni zote zilizoorodheshwa katika soko umepungua kwa Sh bilioni 217 kutoka Sh bilioni20.5 wiki iliyopita hadi Sh Trilioni 20.2 wiki ilioyoishia Novemba 3 mwaka huu na kwamba punguzo hilo limetokana na kupungua kwa bei za hisa za KA (8%), JHL (8%), CRDB (6%) na TBL  (5%).

Amessisitiza kuwa ukubwa wa mtaji wa kampuni za ndani umepungua kutoka Sh bilioni 112 kutoka Trilioni 10.163 hadi kufikia Sh trilioni 10.051 wiki hii ikisababishwa na kupungua kwa bei za hisa za kampuni za CRDB (6%) na TBL (5%).

Amefafanua kuwa mauzo ya hati fungani katika wiki iliyoishia Novemba 3 yalikuwa Sh bilioni 15.7 kutoka Sh milioni 500 wiki iliyopita ya Oktoba 27 mwaka huu.
Ameongeza kuwa mauzo hayo yametokana na hatifungani 11 za Serikali na za Makampuni binafsi zenye jumla ya thamani ya Sh bilioni 15.7.

Pia amesema kiashiria cha kampuni zote zilizoorodheshwa katika soko hilo yaani DSEI kimeshuka kwa pointi 23 kutoka pointi 2,124 hadi 2,101 kutokana na kushuka kwa bei za hisa za Shrika la Ndege la Kenya(KA) Jubilee Holdings ltd (JHL), CRDB na TBL.

Katika hatua nyingine, amesema kiashiria cha kampuni za ndani (TSI) kimepungua kwa pointi 43 kutoka pointi 3,876 hadi 3,833 sababu ya kushuka kwa bei za hiza za CRDB na TBL..

Wakati huo huo, ameanisha kuwa kiashiria cha sekta ya viwanda kimepungua kwa poiti 77 kutoka pointi 5,379 hadi 5,303,  kiashiria cha huduma za kibenki na fedha kimeshuka kwa pointi 33 kutoka pointi 2,497 hadi 2,464 huku cha Sekta ya huduma za kibiashara wiki hii kimebaki kama awali kwenye wastani wa pointi 2,462.

0 maoni:

Chapisha Maoni

Kurasa

Translate

Popular Posts

Blog Archive

Tangazo!

JE UNAHITAJI KUBORESHA BLOG YAKO?

WEIGHT MANAGEMENT

WEIGHT MANAGEMENT

SIKILIZA NYIMBO MPYA

Watembeleaji

On Facebook

Tangazo Victoria!!

Date & Time

Weight Management



CLICK THIS IMAGE

Sikiliza Clouds Radio



Sikiliza Kwanza Jamii Radio

Total Pageviews

Fomu ya Anwani

Jina

Barua pepe *

Ujumbe *