WELCOME TORINTO HOT MEDIA BLOG | FOR MORE INFORMATION ABOUT OUR NEWS CONTACT US CELL: +255 756 188 180 | Email: josephlieme@gmail.com| KARIBU TORINTO HOT MEDIA BLOG | KWA MAELEZO ZAIDI KUHUSU HABARI ZETU WASILIANA NASI SIMU: +255 756 188 180 | Barua Pepe: josephlieme@gmail.com | DO YOU NEED TO DEVELOP YOUR BLOG CONTACT US CLICK HERE | JE UNAHITAJI KUBORESHA BLOG YAKO WASILIANA NASI BOFYA HAPA

Jumatano, 4 Oktoba 2017

 02:29      No comments

Endelea kufuatilia Torinto Hot Blog.

 TAGS


Rais Magufuli akisalimiana na mwenyekiti wa Jumuiya ya tawala za mitaa(ALAT) siku ya leo alipofika kwa ajili ya kufungua mkutano wao wa mwaka

Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli ameahidi kuwafukuza kazi Wakurugenzi wa halmashauri wanne kwa ulevi wa pombe pindi wawapo makazini.

Rais Magufuli amesema hayo alipokuwa kwenye Mkutano wa 33 wa Jumuiya Ya Tawala za Mitaa (ALAT) ambao uliofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Mwalimu Nyerere Dar es Salaam na kusema amepata taarifa kuwa wapo Wakurugenzi kadhaa ambaio ni walevi na kudai wasipobadilika ndani ya muda mfupi atawafukuza kazi.

"Nimepata taarifa ya Wakurugenzi kama wawili watatu hivi ni walevi sana, nawaambia hao wataondoka kama upo hapa Mkurugenzi halafu ni mlevi ukajirekebishe haraka sana, kabla sijaja huko ili angalau uonekane umebadilika" alisema Rais Magufuli.

Mbali na hilo Rais Magufuli aliwataka viongozi hao kwenda kumaliza migogoro mbalimbali ndani ya halmashauri zao na mivutano isiyokuwa na msingi na kusema kuwa vyama vya siasa si adui bali adui wa kwanza wa serikali yake ni watu wanaokuja kuiba maliasili za Tanzania.

"Haipendezi kuwa na makundi, muyamalize makundu hayo kwenye manispaa, tunajenga nyumba moja adui yetu siyo vyama tunachelewa sana, adui yetu ni wale wanaotuibia nasema mkamalize hayo makundi huko, najua tofauti lazima zitakuwepo lakini kwenye masuala ya kazi lazima tushikamane kwa maslahi ya Watanzania, mkawaimize Watanzania kufanya mambo ya maendeleo" alisisitiza Rais Magufuli

0 maoni:

Chapisha Maoni

Kurasa

Translate

Popular Posts

Blog Archive

Tangazo!

JE UNAHITAJI KUBORESHA BLOG YAKO?

WEIGHT MANAGEMENT

WEIGHT MANAGEMENT

SIKILIZA NYIMBO MPYA

Watembeleaji

On Facebook

Tangazo Victoria!!

Date & Time

Weight Management



CLICK THIS IMAGE

Sikiliza Clouds Radio



Sikiliza Kwanza Jamii Radio

Total Pageviews

Fomu ya Anwani

Jina

Barua pepe *

Ujumbe *