WELCOME TORINTO HOT MEDIA BLOG | FOR MORE INFORMATION ABOUT OUR NEWS CONTACT US CELL: +255 756 188 180 | Email: josephlieme@gmail.com| KARIBU TORINTO HOT MEDIA BLOG | KWA MAELEZO ZAIDI KUHUSU HABARI ZETU WASILIANA NASI SIMU: +255 756 188 180 | Barua Pepe: josephlieme@gmail.com | DO YOU NEED TO DEVELOP YOUR BLOG CONTACT US CLICK HERE | JE UNAHITAJI KUBORESHA BLOG YAKO WASILIANA NASI BOFYA HAPA

Jumanne, 4 Julai 2017

 02:56      No comments


 TAGS
Wabunge sita wa Chadema usiku wa kumkia leo wamehojiwa na polisi kwa tuhuma za kumshambulia Mbunge wa Viti Maalum (CCM) Juliana Shonza.

Mwenyekiti mwenza wa wabunge wanaounda umoja wa katiba (Ukawa) James Mbatia amewataja wanaoshikiliwa kuwa ni Mbunge wa Mlimba Suzan Kiwanga, Saed Kubenea(Ubungo), Pauline Gekul (Babati Mjini), Frank Mwakajoka (Tunduma), Joseph Selasini (Rombo) na Cecilia Pareso (Viti Maalum).

Hadi saa 5.00 usiku wabunge hao bado walikuwa wakiandika maelezo katika kituo cha polisi. Wabunge hao ni kati ya wabunge wanane waliotajwa na Spika wa Bunge Job Ndugai alipokuwa akiahirisha kikao cha bunge jioni kuwa wanatuhumiwa kumshambulia Shonza.

Wabunge wengine waliotajwa katika sakata hilo lililotokea Jumatatu mchana mchana katika lango la kuingilia jengo la utawala ni Devotha Minja (Viti Maalum) na Cecil Mwambe (Ndanda).

Hata hivyo James Mbatia alipohojiwa Saa 5.45usiku alisema kuwa wabunge hao waliachiwa kwa dhamana baada ya mahojiano na kutakiwa kurud polisi Jumanne Saa 3 asubuhi.

Hata hivyo Mbatia ameshangazwa na kitendo cha kutajwa kwa Mwambe ambaye amesema hii ni wiki ya pili hayupo mjini Dodoma.

“Mimi nilikuwa msimamizi wa kambi yetu, Mwambe aliniaga tangu wiki mbili zilizopita anaenda jimboni na hajarudi sasa tunashangaa kutajwa alikuwepo wakati wa tukio,” amesema.

Wabunge hao walidakwa mmoja mmoja na askari waliokuwa wamevalia mavazi ya kiraia (askari kanzu) wanaolinda bunge.

Kukamatwa kwa wabunge hao kulifuatia Shonza kwenda kushtaki kwa Ndugai naye kutoa kibali cha kukamatwa kwa wabunge hao.

0 maoni:

Chapisha Maoni

Kurasa

Translate

Popular Posts

Blog Archive

Tangazo!

JE UNAHITAJI KUBORESHA BLOG YAKO?

WEIGHT MANAGEMENT

WEIGHT MANAGEMENT

SIKILIZA NYIMBO MPYA

Watembeleaji

On Facebook

Tangazo Victoria!!

Date & Time

Weight Management



CLICK THIS IMAGE

Sikiliza Clouds Radio



Sikiliza Kwanza Jamii Radio

Total Pageviews

Fomu ya Anwani

Jina

Barua pepe *

Ujumbe *