WELCOME TORINTO HOT MEDIA BLOG | FOR MORE INFORMATION ABOUT OUR NEWS CONTACT US CELL: +255 756 188 180 | Email: josephlieme@gmail.com| KARIBU TORINTO HOT MEDIA BLOG | KWA MAELEZO ZAIDI KUHUSU HABARI ZETU WASILIANA NASI SIMU: +255 756 188 180 | Barua Pepe: josephlieme@gmail.com | DO YOU NEED TO DEVELOP YOUR BLOG CONTACT US CLICK HERE | JE UNAHITAJI KUBORESHA BLOG YAKO WASILIANA NASI BOFYA HAPA

Jumatatu, 17 Julai 2017

 06:29      No comments


 TAGS

Katibu Mkuu wa Chama Cha Alliance for Democratic Change (ADC) Doyo Hassan Doyo ameitaka Mamlaka ya Mapato nchini TRA kusitisha zoezi la kuvifungia vituo vya mafuta nchini kwani limewakosesha huduma watanzania wengi ambao kimsingi hawana hatia na hadha wanayoipata.

Akizungumza leo Jijini Dar es Salaam katika ofisi za chama hicho zilizopo Buguruni Rozana Katibu Mkuu huyo ameeleza kuwa ni vyema serikali ikawachukulia hatua za kisheria wamiliki wa vituo hivyo mafuta na kuruhusu huduma ziendelee kwani huduma ya mafuta imeendelea kuwa mtihani kwa wananchi wa maeneo mbalimbali hapa nchini.

Mamlaka ya Mapato nchini ipo katika oparesheni ya kuvifungia vituo vya mafuta nchini ambazo havijafunga mashine za EFD katika 'Pump ' za mafuta jambo ambalo halichochei ukusanywaji wa mapato wenye ukweli wa takwimu.

Katika hatua nyingine Katibu Mkuu Doyo amesema ADC inakitaka Chama Cha Demokrasia na Maendeleo Chadema Kutoingilia Mgogoro ulikuwepo Ndani ya Chama cha Wananchi CUF.

Ambapo amesema kuwa Chadema kuingilia Mgororo wa CUF kunaweza kuhatarisha amani ya nchi.

"Tumeshuhudia Migogoro mingi ya vyama vya siasa lakini hatujaona kingene kikiingilia Mgogoro wa Chama kingine".

Hata hivyo Doyo ameitaka serikali iviache vyama vya siasa nchini vifanye shughuli zao.

ADC ipo katika maandalizi ya Maadhimisho ya kuzaliwa kwa Chama hicho ambayo yatafanyika Tarehe 22 Agosti Mwaka Huu ambapo chama hicho kitakuwa na ziara kwenye asasi za Kiraia, kuwatembea Wagonjwa, Wafungwa, Vyuo vikuu na Kutembea Nyerere Foundation ,N.K  na Mwisho kuhitimisha kwenye Ofisi za chama hicho Buguruni Jijini Dar es Salaam, huku vyama mbalimbali vikialikwa.

0 maoni:

Chapisha Maoni

Kurasa

Translate

Popular Posts

Blog Archive

Tangazo!

JE UNAHITAJI KUBORESHA BLOG YAKO?

WEIGHT MANAGEMENT

WEIGHT MANAGEMENT

SIKILIZA NYIMBO MPYA

Watembeleaji

On Facebook

Tangazo Victoria!!

Date & Time

Weight Management



CLICK THIS IMAGE

Sikiliza Clouds Radio



Sikiliza Kwanza Jamii Radio

Total Pageviews

Fomu ya Anwani

Jina

Barua pepe *

Ujumbe *