WELCOME TORINTO HOT MEDIA BLOG | FOR MORE INFORMATION ABOUT OUR NEWS CONTACT US CELL: +255 756 188 180 | Email: josephlieme@gmail.com| KARIBU TORINTO HOT MEDIA BLOG | KWA MAELEZO ZAIDI KUHUSU HABARI ZETU WASILIANA NASI SIMU: +255 756 188 180 | Barua Pepe: josephlieme@gmail.com | DO YOU NEED TO DEVELOP YOUR BLOG CONTACT US CLICK HERE | JE UNAHITAJI KUBORESHA BLOG YAKO WASILIANA NASI BOFYA HAPA

Jumatano, 31 Mei 2017

 04:22      No comments


Makamu Mwenyekiti wa TPSF, Salum Shamte akizungumza wakati wa kufungua mkutano wa 17 wa Mfuko wa Sekta Binafsi nchini uliofanyika leo jijini Dar es Salaam.

Mkurugenzi Mtendaji wa TPSF, Godfrey Simbeye akikaribisha wajumbe wa mkutano mkuu wa mfuko huo leo katika uliofanyika katika ukumbi wa Serena jijini Dar es Salaam
Sehemu wajumbe wa Mkutano 17 wa TPSF uliofanyika katika ukumbi wa Serena jijini Dar es Salaam
Mfuko wa Sekta Binafsi Nchini (TPSF) umesema kuwa katika kujenga mazingira ya biashara kunahitaji kuwepo kwa sekta ya umma pamoja na sekta binafsi katika kuandaa maeneo tengefu ya biashara.

Hayo yamebainishwa leo Makamu Mwenyekiti wa TPSF, Salum Shamte kwa niaba ya Mwenyekiti wa TPSF wakati akifungua mkutano wa 17 wa mwaka wa Mfuko wa Sekta ya Binafsi (TPSF) uliofanyika leo jijini Dar es Salaam.

Shamte amesema kuwa katika kuendana na mipango ya kufikia uchumi wa kati sekta binafsi na sekta ya umma zinatakiwa kushirikiana katika kuangalia mazingira ya kufanya uwekezaji wa viwanda. 

Amesema katika maagizo ya Rais Dk. John Pombe Magufuli kwa wakuu wa mikoa , kutenga maeneo ya viwanda ambapo kuna uwezekano huo upo lakini changamoto ni miundombinu ya maeneo hayo.

Aidha ameiomba serikali kuanizisha Benki ya kuendeleza viwanda ili sekta hiyo iweze kukua na kufikia uchumi wa kati kwa kuajili watanzania wengi.

Shamte ameomba serikali kuongeza bajeti kwa mamlaka ya EPZA ili kuweza kutenga maeneo tengefu ya viwanda.


Hata hivyo amesema kuwa sekta binafsi ndio inaajiri kwa sehemu kubwa kuliko sekta ya umma, kutokana na takwimu zinaonesha kwa mwaka vijana wanahitimu 800,000 kwa sekta ya umma inaajiri vijana 40,000. 

0 maoni:

Chapisha Maoni

Kurasa

Translate

Popular Posts

Blog Archive

Tangazo!

JE UNAHITAJI KUBORESHA BLOG YAKO?

WEIGHT MANAGEMENT

WEIGHT MANAGEMENT

SIKILIZA NYIMBO MPYA

Watembeleaji

On Facebook

Tangazo Victoria!!

Date & Time

Weight Management



CLICK THIS IMAGE

Sikiliza Clouds Radio



Sikiliza Kwanza Jamii Radio

Total Pageviews

Fomu ya Anwani

Jina

Barua pepe *

Ujumbe *