WELCOME TORINTO HOT MEDIA BLOG | FOR MORE INFORMATION ABOUT OUR NEWS CONTACT US CELL: +255 756 188 180 | Email: josephlieme@gmail.com| KARIBU TORINTO HOT MEDIA BLOG | KWA MAELEZO ZAIDI KUHUSU HABARI ZETU WASILIANA NASI SIMU: +255 756 188 180 | Barua Pepe: josephlieme@gmail.com | DO YOU NEED TO DEVELOP YOUR BLOG CONTACT US CLICK HERE | JE UNAHITAJI KUBORESHA BLOG YAKO WASILIANA NASI BOFYA HAPA

Jumanne, 21 Machi 2017

 02:10      No comments


 TAGS

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Moses Nnauye ameunda kamati ya watu watano kuchunguza suala la kilichotokea Clouds Media siku ya Alhamisi pamoja na Ijumaa usiku.
Kamati hiyo imeundwa baada ya Waziri Nape kufanya ziara Clouds Media leo Jumatatu 20/03/2017 na kuzungumza na uongozi wa Clouds Media kufuatia tukio la Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam kutembelea ofisi hizo siku ya Ijumaa usiku akiwa na askari wenye silaha.
Kamati hiyo itaongozwa na Mwenyekiti Dkt. Hassan Abbas Mkurugenzi Idara ya Habari MAELEZO, Bw. Deodatusi Balile Makamu Mwenyekiti Jukwaa la Wahariri, Ndg. Jesse Kwayu Mhariri Mtendaji Gazeti la Nipashe, Ndg. Mengida Johannes kutoka Wapo Redio pamoja Ndg. Mabel Masasi kutoka Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA).
Baada ya kamati hii kufanya uchunguzi wa kina na kujiridhisha kutoka pande zote mbili Wizara itasema hatua itakazochukua.  

Imetolewa na:
Zawadi Msalla
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo.

0 maoni:

Chapisha Maoni

Kurasa

Translate

Popular Posts

Blog Archive

Tangazo!

JE UNAHITAJI KUBORESHA BLOG YAKO?

WEIGHT MANAGEMENT

WEIGHT MANAGEMENT

SIKILIZA NYIMBO MPYA

Watembeleaji

On Facebook

Tangazo Victoria!!

Date & Time

Weight Management



CLICK THIS IMAGE

Sikiliza Clouds Radio



Sikiliza Kwanza Jamii Radio

Total Pageviews

Fomu ya Anwani

Jina

Barua pepe *

Ujumbe *